Friday, May 3, 2013

WAKAZI WA BUHARE MANISPAA YA MUSOMA KUPATA FIDIA MWEZI MEI MWAKA HUU KUPISHA UJENZI WA NYUMBA ZA SHIRIKA HILO




 Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Nyumba Tanzania (NHC) Nehemia Mchechu (mwenye kofia) wakiangalia jengo la Jengo la Hospitali ya Rufaa ya Mwalimu Nyerere Memorial Medical  Center iliyopo eneo la Kwangwa Manispaa ya Musoma.


Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Nyumba Tanzania (NHC) Nehemia Mchechu akizungumza na wadau wa Shirika hilo katika ukumbi wa uwekezaji wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara juu ya ujenzi wa nyumba za shirika hiloManispaa ya Musoma.



Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Nyumba Tanzania (NHC) Nehemia Mchechu (mwenye kofia) akiwa na watendaji wengine wa shirika hilo na serikali wakielekea kwenye jengo la Jengo la Hospitali ya Rufaa ya Mwalimu Nyerere Memorial Medical  Center iliyopo eneo la Kwangwa Manispaa ya Musoma.

 


Na Thomas Dominick,

Musoma



WAKAZI wa Buhare Manispaa ya Musoma wapo mbioni kulipwa fidia kutoka kwenye Shirika la Nyumba Tanzania (NHC) kwa ajili ya kupisha ujenzi wa mji mpya wa Musoma.



Hayo yalisemwa na Mkurugenzi mtendaji wa Shirika hilo, Nehemia Mchechu ambaye alikuwa na ziara ya kutembelea mkoa huo aliwatoa wasiwasi viongozi wa Manispaa hiyo kuhusiana na uendelezaji wa mji huo baada ya kuwapatie eneo hilo tangu mwaka 2010.



Nehemia alisema kuwa shirika hilo linatarajia kutoa fidia hiyo mwezi mei mwaka huu baada ya kukamilisha taratibu zote za kufanya tathimini ya nyumba  na maeneo ya wakazi wa eneo hilo.



“taratibu zote za kuwalipa fidia zimekamilika na mwezi ujao (mei) tutaanza kutoa malipo ya fidia kwa wakazi hao ili wapishe ujenzi huo ambao tunatarajia kuanza katika kipindi cha fedha cha mwaka 2013/14,”alisema Mchechu.



Alisema kuwa eneo hilo litatumika kujengwa nyumba za kisasa ambazo zitakuwa kwa ajili ya kupangisha pamoja na kuuza kwa wananchi kwa bei nafuu na kupata makazi bora.



Mchechu alisema kuwa pamoja na eneo hilo la Buhare pia watajenga nyumba zingine katika wilaya za Serengeti na wilaya mpya Butiama kwa ajili ya kumuenzi baba wa Taifa Mwl. Julius Nyerere kwani ndiye mwazilishi wa shirika hilo.



“Pamoja na Buhare lakini tunatarajia kufanya ujenzi katika wilaya mbili ya Serengeti na Butiama na Butiama ni kwa ajili ya kumuenzi baba wa Taifa kwani ndiye mwanzilishi wa shirika letu lazima tumrudishie heshima yake,”alisema.



Naye Naibu Meya Bwire Nyamwero alimtaka Mkurugenzi huyo kufanya zoezi hilo bila kuchelewa kwani wananchi wa Musoma wanasubiria kwa hamu mradi huo na kumuhakikishia kuwa kama anataka eneo jingine atapewa.



“Napenda kumtoa wasiwasi mkurugenzi wa NHC kuwa tupo tayari kupokea mradi huo mkubwa lakini nimuhakikishie kuwa kama anataka eneo jingine aseme tutampatia,”alisema Nyamwero.



Mkuu wa Mkoa John Tuppa alisema kuwa mkoa wa Mara kuna maeneo mengi na makubwa kwa ajili ya uwekezaji hivyo watumie fursa ya Shirika hilo kuwekeza kwa manufaa ya wananchi wao.

M WISHO



Read More...