Sunday, December 16, 2012

MKUTANO WA BULEMBO MUSOMA WACHAFUKA

 *Risasi za moto zarindima polisi wadumisha ulinzi maeneo ya mjini
*Wanne wakamatwa
*Askari Polisi Mmoja ajeruhiwa ashonwa nyuzi tano kichwani

 Gari ya Polisi Musoma ikiwa katika harakati za kutuliza vurugu katika mkutano wa Mwenyekiti wa Jumuia ya Wazazi CCM Taifa Abdalah Bulembo uliofanyika katika viwanja vya Shule ya Mukendo Manispaa ya Musoma.
Askari Polisi wakishuka kwenye gari kwa ajili ya kudhibiti hali ya Amani kwenye viwanja vya shule ya msingi Mukendo wakati wa mkutano wa Mwenyekiti wa Jumuia ya Wazazi CCM Taifa Abdalah Bulembo.

Askari Polisi wakivinjari kwenye viwanja vya shule ya Msingi Mukendo Baada ya kudhibiti Vurugu
Kijana ambaye hakujulikana mara moja jina lake akidhibitiwa na askari Polisi baada ya Kumkamata.

Wananchi wa Manispaa ya Musoma wakiwa wamebaki vinywa wazi baada ya rabusha kati ya Polisi na Vijana Katika viwanja vya Shule ya Msingi Mukendo Manispaa ya Musoma.

Thomas Dominick,
Musoma

HALI ya amani ilitetereka katika Mkutano wa hadhari ulioitishwa na Jumuia ya Wazazi CCM ya wilaya ya Musoma na kuhutubiwa na Mwenyekiti wa Jumuia hiyo Taifa  Al haji Abdalah Bulembo baada ya Jeshi la Polisi kulazimika kutumia risasi za moto kutawanya vijana wanaodaiwa kuwa wafuasi wa Chadema waliokuwa wanataka kuvamia mkutano huo.

Chanzo cha vurugu hizo ni baada ya askari Polisi kujaribu kumdhibiti kijana mmoja kukamatwa akijiandaa kwenda kufanya fujo kwenye mkutano huo katika vurugu hizo mmoja alijeruhiwa vibaya na kupelekwa hospitali ya Mkoa na kushonwa kasha kuruhusiwa.

Mkutano huo uliofanyika katika viwanja vya shule ya Msingi Mukendo Bulembo alisema kuwa wananchi wa Musoma walikuwa na haki ya kuchagua Chadema katika uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 ili waonje machungu ya upinzani.

Alisema kuwa tayari Serikali ipo tayari kuifungia Manispaa hiyo
kuipatia fedha za ruzuku toka Serikali kuu kwa kuwa fedha ambazo
zilitolewa kwa ajili ya miradi ya maendeleo fedha hizo ziliamishiwa
kwenye ujenzi wa Mitaro.

“Fedha ya Serikali kuu inapitishwa na Bunge hairuhusiwi kuguswa au kupelekwa kwenye mradi mwingine kufanya hivyo ni kosa, hapa Serikali kuu ilitoa fedha ya Ruzuku kwa ajili ya ujenzi wa Barabara lakini fedha hizo zimetumika kwa mambo tofauti na Serikali
ilivyoagiza,”alisema Bulembo.

Bulembo alisema kuwa Serikali inaleta Mkaguzi Mkuu wa fedha za
Serikali ili kufanya ukaguzi wa kina kwa fedha za miradi ili kuona
uozo uliopo ndani ya Manispaa hiyo na kuwahakikishia wananchi baada ya muda mchache watasikia kesi zikiunguruma Mahakamani kutokana na Viongozi kutafuna fedha za Umma bila hofu.

Pia alijibu hoja liyotolewa na Viongozi wa Chadema za Mkuu wa wilaya kutohudhuria kikao chao kwa madai kuwa alikuwa katika m,ahadhimisho ya miaka 51 ya Uhuru wa Tanzania yaliyofanyika katika kata ya Nyakato ndani ta Manispaa hiyo.

“Haiwezekani hata siku moja Mkuu wa Wilaya anayeteuliwa na Rais ambaye naye ni Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Wilya kuhudhuria Mkutano wa Chadema wakati yeye ni mwanachama wa CCM napenda niwaambie hiyo haipo na haitatokea kwa Viongozi kama hao kuhudhuria mikutano ya vyama vya upinzani,”alisema.

Alitumia nafasi hiyo kuwaomba Viongozi wa vyama vya siasa kuacha tabia ya kupanda jukwaa na kuanza kumtukana Rais Jakaya Kikwete na kusema kuwa wameshachoka na matusi hao na kuomba jeshi la polisi kwa kiongozi yeyote atakayetumia jukwaa kuktusi rais achukuliwe hatua pamoja na kufikishwa mahakamani.

“Sisi watanzania hatua utamaduni huu wa kijana au mtu kumtukana mzazi wake Rasi ni amir Mkuu wa majeshi ya Ulinzi na Usalama hapaswi hata siku moja kumtukana hii ni kumkosea adabu na tunapenda kuwaambia jeshi la polisi kuwakamata wote wenye mchezo huu na kuwafikisha mahakamani,”alisema.

Alisema kuwa CCM imekuwa ikitumia majukwaa ya siasa hasa mikutano ya Siasa kwa ajoili ya kurekebisha mapungufu ambayo yanaonekana na wapinzani kitu ambacho kinaendelea kushika hatamu ya uongozi nchini.


Mwisho

1 comment:

  1. mkuu wa wilaya ni mtumishi wa umma na sio wa chama,hayo ni makosa ya kikatiba tu ila in reality hana chama akiwa kazini! ubaya hao watu bado wanadhani musoma watu hawajaenda shule ndo maana wanawadanganya! mitaro c ni sehemu ya barabara au ye hilo halijui? ukijenga barabara bila mtaro unategemea nn?! kwakweli huyu bwana hajajua anachokiongea tu!

    ReplyDelete