Thursday, August 22, 2013

WANANCHI WA KATA YA KIAGATA WILAYA YA BUTIAMA MKOA WA MARA WAOMBA JIMBO LIGAWANYWE, MILONI 420 ZA MADENI ZAWAGAWA MADIWANI

MKUU WA MKOA WA MARA JOHN TUPPA AKIMKABIDHI KAIMU MKURUGENZI RICHARD MIHAYO HATI YA KUDHIBITISHWA KWA HALMASHAURI MPYA YA BUTIAMA ILIYOZALIWA KUTOAKA HALMASHAURI YA MUSOMA.
MKURUGENZI MPYA WA HALMASHAURI YA BUTIAMA RICHARD MIHAYO AKIWA PAMOJA NA HATI YA UANZISHWAJI KWA HALMASHAURI HIYO.


 Na Thomas Dominick

 Butiama



 WANANCHI wa Tarafa ya Kiagata Wilaya ya Butiama, Mkoa wa Mara wameiomba Serikali kuipatia Kata hiyo  jimbo linalojitegemea kutokana na  jimbo la Musoma Vijijini linalotawaliwa na Mbunge Nimrod Mkono kuwa kubwa na kushindwa kufikisha huduma muhimu kwa wananchi.



 Akitoa hoja hiyo katika kikao maalum cha uvuvunjaji wa Halmashauri hiyo na kuzaa Halmashauri mpya ya Butiama, Diwani wa Kata ya Buswahili, Tarafa ya Kiagata Kawaki Marwa  alisema kuwa kutokana na ukubwa wa eneo hilo imekuwa vigumu kuwafikishia huduma muhimu kwa wakazi wa maeneo hayo kufika.



 “Mheshimiwa Mwenyekiti eneo la Kiagata ni kubwa sana, tunaomba sisi kama wananchi wa maeneo hayo Serikali ilikate jimbo hilo na tuwe na majimbo mawili ili kuweza kuwafikishia huduma wananchi kirahisi kuliko ilivyokuwa sasa,”alisema Marwa



 Alisema kuwa Tarafa hiyo ina kata nne na wakazi 35,274 kwa takwimu za sensa iliyofanyika mwaka 2012, nchi mzima kitu ambacho kimesababisha huduma zinazotolewa na mbunge huyo kuwa zinawanufaisha wananchi wa upande mmoja na upande mwingine kuteseka.



 Naye Mkuu wa Mkoa huo John Tuppa wakati akitoa hotuba kabla

 ajakadhidhi hati ya kuashiria uanzishwaji wa Halmashauri hiyo mpya ya Butiama kwa Kaimu Mkurugenzi Richard Mihayo alisema kuwa Halmashauri ya Musoma ina eneo kubwa hivyo inahitaji kupata majimbo mengine mawili.



 “Changamoto zilizokuwa zinaikabili Halmashauri hii ni ukubwa wa eneo na hapa tumeanza tu kugawa katika Halmashauri mbili lakini inatakiwa iwe na majimbo aidha matatu ya uchaguzi ili kuweza kuwaqfikishia huduma wananchi wa maeneo hao,” alisema Tuppa.



 Alisema kuwa pamoja na hilo viongozi wa Halmashauri hizo waache utendaji kazi wa mazoea ili waweze kuwatendea haki wananchi wao ikiwa pamoja na kuwatatulia kero mbalimbali zinazowakabili.



 Ugawaji wa Halmashauri hizo ilifanyika ikiwa ni pamoja na kugawana raslimali na madeni yaliyokuwepo katika Halmashauri hiyo hatua hiyo ambayo ilikwisha kwa amani na utulivu huku kila mjumbe akiridhia ugawaji huo.



 Hivi karibuni katika mchakato kama huo wa kugawa Halmashauri ya Tarime na Halmashauri ya Mji wa Tarime vurugu zilitokea kutokana na madiwani watatu wa viti maalumu wa CCM na Chadema kukataliwa kuingiwa Mjini kwa madai hawakai maeneo ya mjini na kusababisha kutoelewana na madiwani kurushia maneno na kuvunjiaka bila muafa.



 MWISHO











 Na Thomas Dominick

 Butiama.



 HALMASHARI ya Wilaya ya Musoma Mkoa wa Mara imejikuta katika wakati mgumu pale baada ya madiwani kuitaka halmashauri kutoa ufafanuzi wa kina juu ya malimbikizo ya madeni kubwa la Milioni 402 ambazo zimeweza kusababisha kuzorota kwa  suala zima la Maendeleo kwa wananchi.



 Wakichangia hoja mbalimbali hii leo katika  kikao maalum kilichokuwa na lengo la kujadili mgawanyiko wa rasirimali kati ya halmashauri ya wilayaya  Musoma pamoja na Butiama, Diwani wa kata ya Nyambono Grayson Mfungo amesema kuwa  malimbikizo ya milioni 402 ni mzigo mkubwa kwa Halmashauri kitendo ambacho kinaweza kukwamisha baadhi ya shuguli za kimaendeleo.



 Kambi ya upinzani walitaka kujua halmashauri ilikuwa wapi mpaka

 inafikia hatua ya malimbikizo kwa watendaji  wanaokaimu idara mbali mbali na kudai kuwa watakubaliana  na mgawanyiko wa raslimali endapo tu halmashauri itatoa majibu ya kuridhisha kuhusiana na suala hili.



 Akijibu hoja hiyo Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Musoma Fidelica Myovela, alikiri kuwa  halmashauri inakabiliwa na deni kubwa na sehemu kubwa ya deni hilo nikutokana na posho za kukaimu nafasi ya Ukuu wa Idara  ambapo zilistahili kulipwa kwa wakuu mbalimbali wa idara.



 Naye Mkuu wa Mkoa wa huo,  John Tuppa  alikiri kupokea taarifa za malimbikizo ya madeni na  amehaidi kulipeleka suala hilo katika

 serikari kuu sambamba na uwasilishwaji wa wakuu mbali mbali wa idara ili kuweza kuondokana na tatizo la ukaimu ambapo limekuwa

 likisababisha mzigo mkubwa Kwa halmashauri.



 Aidha alizitaka halmashauri  kuhakikisha kuwa zinaboresha  mapato yake ya ndani na kuziba mianya yote inayopita fedha hizo katika mifuko ya watu binafsi ili  kuepuka ongezeko la msaada wa kifedha kutoka serikali kuu.



 “Viongozi wanashindwa kusimamia sheria za ukusanyaji mapato na hicho ndicho chanzo cha upotevu wa mapato ya ndani utakuta viongozi wana vitabu bandia vya risti za kukusanyia fedha za serikali, viongozi kama hawa hawatufai,”alisema Tuppa.



 Halmashauri ya wilaya ya Musoma imeweza kujitenga rasmi na kuzaa wilaya mbili  Butiama pamoja na Musoma Vijijini inayopigiwa debe iitwe kwa jina Nyanja lengo kuu likiwa kurahisisha huduma kwa wananchi.





 MWISHO


0 comments:

Post a Comment