Thursday, December 20, 2012

BODA BODA WA MANISPA YA MUSOMA ACHINJWA WILAYANI BUTIAMA








 Wananchi na waendesha Pikipiki wa Manispaa ya Musoma wakiwa wamefurika kumuona marehemu Thomas Majengo Mtaa wa Kiara ambaye amechinjwa shingo kwa nyuma na kukatwa mguu wake wa kulia na watu wanaodaiwa kuwa majambazi katika kijiji cha Kisamwene Kata ya Butuguri wilaya ya Butiama kisha kunyang'anywa pikipiki yake.
 Waendesha Pikipiki wakiwa nje ya Hospitali ya Mkoa wa Mara wakiwa wamepigwa butwaa baada ya mwenzao Thomas Majengo mkazi wa Mtaa wa Kiara ambaye amechinjwa shingo kwa nyuma na kukatwa mguu wake wa kulia katika kijiji cha Kisamwene Kata ya Butuguri wilaya ya Butiama kisha kunyang'anywa pikipiki yake.

 Mwaendesha Boda Boda wakitoka Hospitali ya Mkoa wa Mara na kuelekea nyumbani kwa marehemu Thomas Majengo Mtaa wa Kiara ambaye amechinjwa shingo kwa nyuma na kukatwa mguu wake wa kulia katika kijiji cha Kisamwene Kata ya Butuguri wilaya ya Butiama kisha kunyang'anywa pikipiki yake.


 Daktari akimfanyia vipimo Marehemu Thomas Majengo ambaye ni mwendesha Pikipiki maarufu Boda boda Mkazi wa Kiara Kigera Manispa ya Musoma Baada ya kuchinjwa shingo kwa nyuma na kukatwa mguu wake wa kulia kisha kunyang'anywa pikipiki yake.




Na Thomas Dominick,
Musoma

KIJANA aliyetambuliwa kwa jina la Thomas Majengo (23-28) Mkazi wa Kiara Manispaa ya Musoma Mkoa wa Mara amechinjwa shingo kwa nyuma na kukatwa mguu wake wa kulia na kunyang’anywa Pikipiki na watu wanaodaiwa kuwa majambazi.

Tukio hilo lilitokea Desemba 19 mwaka huu saa 2:30 usiku ambapo inadaiwa kuwa mwendesha Pikipiki huyo alikodiwa na watu ambao hawajajulikana ili awapeleke Katika Wilaya ya Butiama katika kijiji cha Kisamwene Kata ya Butuguri.

Jeshi la Polisi lilipata taarifa la tukio hilo na kwenda kuchukua mwili wa marehemu ambapo baada ya kufika Mjini Musoma waendesha pikipiki wote waliandamana na hadi kufika katika hospitali ya Mkoa huo hali iliyosababisha usumbufu na hofu kwa watumiaji wengine wa barabara.

Mwandishi wa habari alifika kwenye ofisi ya Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa,  Japhet Lusingu  ambaye alisema kuwa hawana tarifa na tukio hilo na kusema kuwa kam kuna sehemu nyingine ya kwenda kuchukua taarifa basi mwandishi huyo afuatilie.

“Sisi hatujui chochote kile kama kuna sehemu nyingine ya kwenda kuchukua taarifa basi nenda,”alisema Lusingu.

Ilibidi mwandishi huyo aende Ofisi ya Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa, Dokta Iragi Ngerageza ambapo alisema kuwa naye hajapata tukio kama hilo hivyo kuahidi kufuatilia kutokana na kuwa taarifa aliyopata ni matukio mengine.

Safari haikuishia hapo kwa mwandishi ndipo alipokwenda hadi katika chumba cha kuhifadhia maiti ya Hospitali hiyo ambapo alikutana na muhudumu wa jingo hilo aliyejitambulisha kwa jina la Masatu ambaye alikubali kutoa ushirikiano na kutaja jina la marehemu.

MWISHO

0 comments:

Post a Comment