Friday, March 29, 2013

WAKRISTO WA SASA TUNAJIFUNZA NINI KUTOKANA NA MANENO SABA ALIYOSEMA YESU MSALABANI SIKU YA IJUMAA KUU

YESU ATUNDIKWA MSALABANI AKIWA NA WAALIFU WAWILI
 YESU AUBEBA MSALABA WAKE KUELEKEA GOLGOTA KUSULIBIWA KWA AJILI YA DHAMBI ZA WANADAMU

Na Thomas Dominick
Musoma
Wayahudi walipomkamata Yesu walimtesa sana kuanzia usiku hadi asubuhi ya siku ya pili kisha alivishwa taji la miiba kichwani na mwanzi mkononi wake wa kuume pia wakati anapelekwa kusulubiwa alibebeshwa msalaba mzito ambao ulimuelemea.(Yohoha 27:29)

Alipofika sehemu iliyokuwa inaitwa golgatha yaani "Fuvu la kichwa" Yesu alivuliwa nguo zake na kumpigilia misumari mikononi na miguuni kisha kutundikwa msalabani.(Luka 15:22)

Padri John Mlekano wa Kanisa la Anglikana Tanzania anafafanua kiundani juu ya maneno saba ambayo Yesu Kristo aliyasema baada ya kutungikwa msalabani siku hiyo ya Ijumaa Kuu.

Pia anasema kuwa kwa maneno hayo wanadamu wanapaswa kuyatekeleza yale ambayo yanamlenga moja kwa moja sababu yanaweza kumsaidia katika maisha yake ya kidunia na kuishi katika maisha ya utakatifu.

Padri Mlekano anasema kuwa wakati Yesu ameangikwa msalaba alitoa jumbe mbalimbali ambapo alitoa maneno ya msamaha, usia, maneno ya maombi, maneno ya kuombea wengine, maneno ya maumivu yake mwenyewe.

"Maneno haya saba yalikuwa ni kauli zake za mwisho kabla hajakata roho ambapo katika maneno hayo saba hayakulenga kwa wanafunzi wake tu bali mengine yalikuwa kati yake na Mungu na hata yule mwalifu aliyeomba toba."alisema.


Neno la kwanza baba wasamehe maana hawajui watendalo (Luka 23:34)
Katika maneno haya yanawafundisha wanadamu wa leo kutoa msaamaha kwa mtu ambaye amekukosea na kukuudhi kwa namna yeyote ile lazima umsamehe kwa kuwa inawezekana hajui nini anakifanya kwa muda huo.

"Kwa maneno haya yanatugusa sisi moja kwa moja kutokana na dhambi zote tunazozifanya hapa ulimwenguni Mungu anakubali kutusamehe lakini baada ya kusamehewa tuna wajibu fulani wa kuutimiza kwake pamoja na kuomba toba."alisema. 

Alisema kuwa kwa somo hilo hapaswi mwanadamu kufanya makosa kwa makusudi kwa kuwa Mungu atamsamehe ila kama imetokea kwa bahati mbaya unatakiwa kufanya toba ya kweli na kutorudia tena kama yule mwalifu aliomba toba akiwa msalabani.


Amini nakuambia leo hii utakuwa nami mahala pema peponi 
 (Luka 23:43) 

Hapa Inaonyesha kuwa Yesu anatangaza ufalme wake katika, mazingira yale aliyoonekana kama mtu jambazi au mwalifu lakini wapo waliomuona kwa macho tofauti ya kuwa hakuwa mwalifu na hata mwalifu alikiri na kumuomba Yesu ampokee kule waendako.

Yule mwalifu alisema ‘EE Yesu nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako, na yesu akamwambia amini nakuambia leo leo hii utakuwa nami peponi.’(Luka 23:42-43) mwalifu yule aliyasema haya kwa kumtambua kuwa yeye ana mamlaka mbinguni hii inaonesha wote walikuwa na nafasi sawa ya kuomba msaamaha lakini mmoja alifanya kashifa na mwingine aliomba msaamaha. 

"Huu ni mfano wa kuigwa kwa maisha yetu ya leo maana inatuonesha yule aliyekashifu hakuona utukufu wa Mungu ila wa pili alisema kuwa sisi tunasitahili adhabu lakini huyu hakufanya kosa lolote na kitu cha kuigwa zaidi ni kutoka kwa yule mwalifu alifanya booking katika ufalme."alisema.

Aliongeza kuwa katika dunia hii wapo wanaoukataa ukuu wa Mungu ingawa upo katikati yetu na kutokubali kabisa kuutumia na wapo wanaouona na kuutumia.


Mama tazama mwanao mwana tazama mama (Yohana 19:26)

Huu ni usia ambao Yesu aliuacha kwa mwanafunzi wake na mama yake kwa sababu hapo alikuwa katika hali kama mwanadamu wa kawaida ambaye yupo katika hali ya kuondoka katika dunia hii anaacha mazingira ya namna gani huku nyuma kwa wanafunzi wake na mama yake.

"Alitambua kuwa wanafunzi wake walimtegemea yeye kwa kila jambo ila aliwaachia ujumbe huo unaowataka watunzane, mshikamane na wasimuangalie yeye kwa kipindi kile ambacho aondoka."alisema.

Lakini Yesu kwa neno hili anawataka wanadamu wasikate tamaa maana watu wengi wanapoondokewa na wale watu muhimu katika maisha yao wanakata tamaa kabisa ila yeye anawataka waendelee kwa jinsi ile alivyokuwa alipowaacha hadi siku ambayo wanadamu wote watakapokutana nao katika ufalme wake.


Mungu wangu Mungu wangu mbona umeniacha (Mathayo 27:46)

Katika maneno haya tunapata fundisho kabla Yesu hajasulibiwa msalabani tulimbebesha mzigo mkubwa wa dhambi zetu kama kafara ateswe na wanadamu wapate kupona.

"Aliwekwa msalabani kama mwalifu, mtenda dhambi ama mtu wa kawaida lakini kiumungu alichukua uovu wetu wote na kwa namna hiyo hakuwa karibu na Mungu katika hali ile anausikia ule uchungu wa kibinadamu."alisema.

"Kwa sababu sisi wakristo tunaamini yesu alikuwa Mungu asilimia mia na mwanadamu asilimia mia kitu ambacho ni kigumu kidogo kwa kumueleza kwa mtu asiyekuwa mkristo haya ni mambo ya imani."aliongeza.

Hivyo katika mazingira yale pale msalabani Yesu hana uungu huwezi kusema kwamba mungu amesulibiwa aliyesulibiwa pale ni Yesu katika nafsi yake ya uanadamu yaani mwanadamu kwa asilimia mia kama unavyojua katika mazingira kama hayo mtu kukosa msaada katika mazingira magumu kama yale lazima ulalamike.

Kwa Hali hii Yesu anamlilia Mungu hili ni ombi lake yeye na Mungu ya kwamba anajisikia yupo mpweke anamlalamikia Mungu kwa nini amemuacha wakati kipindi chote alikuwa karibu naye. 

"Sasa basi fundisho linakuja kwetu sisi kuwa ukipatwa na shida usikimbilie kwenye njia ya mkato kama vile kwenda kwa waganga wa kienyeji au kumtegemea mwanadamu mwenzako kwa jambo ambalo mungu pekee ndiye anayetakiwa kupelekewa shida zako zote, tujue kuwa tuna mtetezi wetu ni Yesu ambaye anaweza kumaliza shida zetu."alisema.

Alisema kuwa kama umeumizwa katika jambo fulani mpigie Mungu magoti umweleze shida yako pale, usiende kuagua, usikimbilie kutoa au kupokea rushwa au kuiba na kusema nina njaa sasa ngoja nikaibe au mbona watoto wamefukuza shule ngoja nikafanye ukahaba nipate hela ya chapu chapu.

"Tusiende kwenye dhambi ila tukimbilie kwanza kwa Mungu tukiwa katika furaha ama katika huzuni yeye ndiye wa kumlilia hicho ndicho tunachojifunza kutoka katika neno hili."alisema.

"Bwana Yesu pale hakulalamika kuwa Mfalme Kaisari mbona mimi nateswa hapa au Pilato kwa nini umeruhusu nisulibiwe au wanafunzi mbona mmeniacha hakuzungumza habari yeyote iliyoonyesha kuwa anamtegemea mwanadamu lakini alionesha kuwa katika shida yake Mungu ndiye aliyekuwa mbele yake na anayeweza kumsaidia katika mateso yake."alifafanua.


Naona Kiu (Yohana 19:28)
"Kiu hii aliyoiona ni kutokana na hali ya uchovu tukumbuke pale yupo katika nafsi ya binadamu na ameteswa usiku kucha tangu jana jioni amepita akiburuzwa na mchana wote jua, msalaba, viboko na miiba lazima atajisikia kiu."alisema. 

Aliongeza kuwa "hapa kuna namna mbili ya kiu ile ya maumivu ya kimwili ambao sasa anasikia mwili unahitaji maji na kiu nyingine inayotafsiriwa kiroho ni kiu ya kuwa na hamu ya kuukomboa ulimwengu nina kiu na hawa watu kwamba wote wangejua kilichonifanya mimi kuja duniani ni kwa ajili yao ninapoondoka watakuwa pamoja nami au watapotea tena."alisema. 


Imekwisha (Yohana 19:30)

Neno hili alilisema baada wale askari kumpelekea chombo chenye siki ili anywe na amalize ile kiu aliyokuwa anaiona lakini baada ya kuipokea alisema kuwa Imekwisha ni neno tu la kukataa kuwa siki yenu sina haja nayo ila kile kilichokuwa rohoni na kilichonileta hapa Duniani nimekimaliza. 

"Fundisho tunalipata ni kuwa baada ya kazi mzito iliyokuwa imemleta Yesu katika ulimwengu huu ameimaliza sasa kazi iliyobaki kwetu wanadamu ni kushika imani na kumkiri kuwa ndiye mwokozi wetu na tukifanya hivyo tutakuwa tumefungua milango yote ya mbinguni na kuingia na kuishi huko kwa raha."alisema.


Baba mikononi mwako naiweka roho yako (Luka 23:46)

Baada ya kufanya kazi ngumu duniani ya kuwatafuta na kuwakomboa wanadamu na kupelekwa msalabani na kuona ametimiza kile alichotumwa na baba yake anasalimisha roho yake kwa kuiondoa ili apumzike na kuikabidhi kwa baba yake.

                       
"Hili nalo ni somo ambalo tunafundishwa kuwa kabla hatujalala tuwe na desturi ya kupiga magoti na kumwambia Mungu kuwa sasa naingia katika hali ya kutojitambua roho yangu hii naikabidhi mikononi mwako usipoamka ipo salama na ukiamuka nayo ipo salama."alisema.

Padri Mlakano anasema kuwa kutokana na somo hilo watu wajenga tabia ya kufanya sala kabla ya kulala, tujue kuna mtu mwenyewe ambaye anamiliki vitu vyote na kila kitu ni chake ina maana kama ukifa hiyo roho haifi inarudi kwa aliyeileta mwili unakwenda kutupwa, roho ni kitu cha thamani ambacho muda wote kinatakiwa kuwa katika hali ya uangalizi wa mwenye chake (Mungu). 

"Hapa utagundua miili yetu ni kama bagi maana wewe ukisafiri nguo zako unazifua na kuweka katika bagi na kwenye gari wanaweza kuliweka kwenye buti lakini mwisho wa safari yako unachojali ni nguo zako zipo salama. Ina maana hii miili ni kasha tu ambapo Mungu ameweka kilicho chake ambayo ni roho."alisema.

Padri Mlekano anamaliza kwa kusema kuwa yote tuliojifunza katika maneno saba aliyosema Yesu msalabani kuwa yote ni mafundisho ya namna fulani ambapo ujumbe wake unaweza kuupokea.

Lakini sio kama maagizo au amri kuwa tuyafuate bali ni vielelezo tu na ujumbe na kwamba kama utausikia utajua namna gani utaenenda katika ulimwengu huu uliojaa kila aina ya dhambi.

MUNGU AKUBARIKI UDUMU KATIKA NENO LAKE MILELE AMINA
0716 000447 / 0767 000448
Read More...

-Ijumaa Kuu : Kubusu Msalaba ni Kuabudu au Kuheshimu?

Na Thomas Dominick


LEO ni siku ya Ijumaa Kuu Wakristo nchini wanaungana na wakristo wenzao Duniani kote kwa kuadhimisha siku ya mateso ya Yesu Kristo Msalabani siku ambayo wanaitumia kama siku ya kumbukumbu ya mateso na kufa kwa mwokozi wao Bwana Yesu Kristo ambaye aliletwa na Mungu ili kuja kuukomboa ulimwengu uliojaa dhambi.

Ijumaa Kuu hutumika kwa maadhimisho ya mambo mengi sana ambayo wakristo wanayafanya katika siku hii pamoja na kufunga na kubusu msalaba ila Ijumaa Kuu hii tutakaloliangalia ni kuhusu msalaba kitendo cha kuubusu ni kuuabudu au kuuheshimu.

Ili tuweze kuelewa vizuri lazima tujue ibaba ni nini na kuna mambo gani yanahitajika katika ibada na kinachotusumbua wengi ni kushindwa kutofautisha kati ya ya kuheshimu na kuabudu.

Kwa maana hiyo maana ya Ibada ni utaratibu uliowekwa na kundi la watu kwa ajili ya kufanya sala na maombi kwa ajili ya kuabudu mbele ya yule anayeabudiwa na watu husika na huyo ndiye Mungu wa kweli mbele yao.

Utashangaa nikisema kuwa Mungu huyo anaweza kuwa jua, jiwe, mti au chochote kile kilichoandaliwa na watu husika jambo kubwa nikuhakikisha shida zao zinapokelewa na kufanyiwa kazi na kujibiwa kama walivyotarajia.

Kwa hiyo penye ibada pana mungu yaani kile kinachoabudiwa na ili ikamilike na kuitwa ibada kuna mambo saba yanahitajika navyo ni Kuheshimu, kutukuza, kuabudu, kutoa sadaka, kusujudu, kusifu na kushukuru.


Kubusu.

Neno Kubusu lina maana nyingi tofauti kutokana na kila Taifa likiwa na tafsiri yake lakini kuabudu ni ishara au dalili ya upendo, Heshima na Furaha.

Biblia inatuambia kuwa hata wakristo wameagizwa wasalimiane kwa busu takatifu (2 Wakorintho 13:12) na tunaona viongozi mbalimbali wanapokutana wanakumbatiana na kubusiana kadhalika hata wazazi huwabusu watoto wao wachanga ili kuwafurahisha.


Kuabudu.

Neno kuabudu maana yake kuwa mtu au watu wanakisujudia au kukitukuza kitu fulani na kupeleka shida zao na kwa madai kuwa watapona au kupata faraja kutoka pale wanapozipeleka shida zao kwa yule wanayemuabudu na kutegemea kuwa matatizo yao yataisha kupitia kwake.

Mfano kila mmoja duniani anamuabudu yule anayedhani ni Mungu na Mitume wake kutokana na imani za kila mtu kwa kupelekea shida zake kwa njia mbalimbali na kujua yeye pekee ndiye atakayemsaidia katika matatizo yake.


Kuheshimu.

Heshima inayozungumzwa katika makala hii ni ile ya kujishusha na kumwinua Mungu. si heshima ya juu juu tu, bali ni heshima yaenye 'ADHAMA'. Ndani yake kuna adhimisho. Adhama maana yake ni ukuu na enzi. Tunapomwadhimisha Mungu, tunaweka juu yake heshima, ukuu, mamlaka na utukufu kuwa ni yeye tu anayestahili kuwa navyo. (1 Nyakati 16:27, Mithali 8:18).


Je Kubusu Msalaba ni Ibada ya sanamu?

Inaonesha kuwa Mungu ndiye aliyekataza ibada ya sanamu na wakati huo huo Mungu alimuagiza Musa atengeneze sanamu ya nyoka wa shaba kule jangwani.


"Bwana akamwambia Musa, jifanyie nyoka wa shaba ukaiweke juu ya mti, na itakuwa kila mtu aliyeumwa, aitazamapo ataishi. Musa akafanya nyoka ya shaba, akaiweka juu ya mti. (Hesabu 21: 4-9)


Baada ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo inawafanya wakristo kujua kuwa Yesu ndiye nyoka wao wa shaba. Na ukimtazama yesu juu ya mti wa msalaba, utapona majeraha yako yote uliyotiwa na shetani. Yeye anakualika akisema;

"Niangalie mimi mkaokolewe, enyi nchi zote za dunia, maana mimi ni Mungu, hapana mwingine." (Isaya 45:22).


Pia Mtume Paulo naye anawaambia wakolosai kuwa,

"Basi vivifisheni viungo vyenu vilivyo katika nchi, uuasharati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya na kutamani, ndiyo ibada ya sanamu." (Wakolosai 3:5).


Kumbe, matendo maovu ndiyo namna ya kisasa ya ibada ya sanamu. Ni bure kuendelea kufikiri kuwa kubusu msalaba ni kuabudu sanamu. Wakristo lazima waelewe kinachosema.
Siku zote maadui wa ukristo wamekuwa wakijaribu kupotosha imani ya asili na kuleta mafundisho yenye kutia mashaka mioyoni mwa waumini. Wasipotambua hayo, watakuwa watu wa kuyumbishwa siku zote katika imani.


Ibada ya sanamu.
Tangu mwanzo Mungu alichukia sana ibada ya sanamu. wapinzani wa imani ya makanisa ya Kikatoliki na Kiapotoliki wanaitumia sababu hii kupinga taswira ya msalaba.

Amri ya pili inasema hivi.

'Usijifanyie sanamu ya kuchonga wala mfano wa kitu chochote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini majani chini ya dunia, usivisujudie wala kuvitumikia....'(Kutoka 20:4-5).


Jambo la muhimu la kuangalia hapa ni kuwa, Mungu hakukataza kutengeneza sanamu. Maana maarifa ya watu wa zamani zile,utengenezaji sanamu ilikuwa ni sanaa ya kawaida kama vile sisi leo tunavyojivunia picha za kamera. katika amri hii Mungu anakataza; Kuvitumikia na Kuvisujudia.


Sanamu ya Yesu ina maana gani leo?

Hili ni swali muhimu sana. Lakini hebu tufikirie kidogo, kama kizazi chetu hiki cha leo kisingeona kumbukumbu ya picha ya Yesu msalabani, bila shaka wengi wasingejua jinsi ile Kristo alivyosulubiwa.

Basi Msalaba ni kielelezo, ni mfano tu, ni taswira ya kutufundisha hata twaweza kujua kwa urahisi jinsi ile mkombozi wetu alivyoangikwa juu ya mti wa ule wa msalaba. 


Kubusu msalaba kama tendo la ibada

Nimekwisha kusema hapo juu kuwa kuheshimu ni sehemu tu katika matendo saba yanayotafsiri ibada. Katika 'Misale ya Waumini' ya kanisa katoliki uk. 245 - 247, kubusu msalaba linaelezwa kama tendo la ibada. 

Nami sina ugomvi na jambo hilo. Maana sioni ubaya wowote endapo msalaba utaabudiwa. Kwa sababu msalaba umekuwa nyenzo muhimu sana katika kuukamilisha wokovu wetu. Pasipo msalaba hakuna wokovu.


Kwa nini Tunabusu msalaba.

Kama tulivyoona hapo juu kuwa busu ni upendo, heshima na furaha, basi kila Ijumaa Kuu tunaonyesha kwa vitendo jinsi tunavyompenda na kumheshimu mwokozi wetu Yesu Kristo kwa kubusu msalaba wake.

Maana ni katika huo ukombozi wetu unapatikana, wala si ajabu, kumbuka yule mwanamke aliyekuwa anatoka damu hakumgusa Yesu bali aligusa pindo la vazi lake tu na akapona na msiba wake (Marko 5:25-34).

Mtu wa Mungu wa kweli aliyekombolewa kweli hujiona mtupu kabisa anapofika mbele ya msalaba. Hii ni kutokana kwamba, kila aliyeokolewa ni kupitia msalaba tu. Ni hatari kuuukata msalaba, hiyo ni dalili ya wazi ya kupotea.

Mtume Paulo alipoongozwa na Roho Mtakatifu alipata kusema: 'Kwa sababu neno la msalaba kwao wanaopotea ni upuuzi, bali kwetu sisi tuliookolewa ni nguvu ya Mungu. (1 Wakorinto 1:18).

Unapobusu msalaba, kumbuka unataka kumwambia Bwana Yesu kuwa, 'Bwana asante kwa kazi yako iliyogharimu maisha yako ili mimi nipate uzima wa milele. Tena tunataka kufanana na mariamu, aliyebusu miguu ya mkombozi wake.(Luka 7:38)

Yaani, inaonesha unyenyekevu wetu kwake na kuikubali kwa moyo ile kazi kubwa asiyo na kifani aliyotutendea. Basi nataka ufahamu kuwa thamani ya msalaba ni ya juu mno kuliko vile ulivyokuwa unafikiri.


Je kuna Faida gani iliyopo kwa kubusu msalaba

Katika maandiko matakatifu inaonesha kuwa kuna faida nyingi sana kwa kuubusu msalaba maana umeponya wagonjwa. Kwa historia ya miaka hiyo tunaona Mt. Herena ndiye aliugundua msalaba wa Yesu huko Yerusalemu mnamo AD 326 baada ya kubomoa jingo na kuchambua ambapo alipata misalaba mingi lakini hakujua upi wa Yesu.

Ili waufahamu kuwa msalaba wa Yesu, Askofu wa Yerusalemu aliamuru aletwe mgonjwa akaugusa mmoja wa misalaba akapona wakajua kuwa ule ndio wenyewe. Msalaba huo uliheshimiwa sana hata ukawekwa katika kanisa kuu la Yerusalemu hadi AD 614 ambapo Waajemi waliuteka.

Lakini uliokolewa na Augusto Heraklio, na ulitekwa tena na Waislamu mwaka 636 AD hii inaonesha kuwa msalaba una faida nyingi kama ukiubusu au ukiushika.


Je msalaba unaweza kukubadilisha ufanane na Yesu

Msalaba ulimbadilisha Dismas yule haramia na kibaka mashuhuri na akashangilia wokovu siku ile ile.


Nguvu iliyomo katika Msalaba.

Tangu siku ya Ijumaa Kuu ya kwanza pale Golgotha, mpaka leo msalaba haujapoteza nguvu zake uliwaokoa wengi, leo upo kwa ajilii yako usiukimbie, ukaribie usiuonee haya ukumbatie usiuache, ubebe.


Piga alama yake tu kifuani mwako nao utakulinda wapo wanaoona kinyaa hata kupiga alama ya msalaba. Msalaba ni mlinzi wako hodari.

Nazungumzia nguvu iliyomo ndani ya msalaba kuwa una uwezo wa kufufua na ukifufuka hufi tena neno kuu kwa ajili yako leo ni uheshimu, upende, ufurahie msalaba maisha yako ya rohoni yatabadilika.


Shika sana ulichonacho

Tatizo kubwa linalolikumba kanisa kwa sasa ni wingi wa mafundisho na waalimu wanaotofautiana toka imani hata imani. Siku hizi kuna imani huria zinazotokana na dhana ya uhuru wa kuabudu.

Tulipofikia sasa si imani tena katika Roho Mtakatifu bali ni fujo na vurugu, hali ya unyenyekevu inapuuzika kila mmoja anataka afanye anavyoona machoni pake. yaani mtu akitofautiana na kiongozi wake hata katika mambo ya kawaida anajitenga na kuunda kanisa.

Wakristo wengi sasa wanajitenga na imani ya kweli na kujiunga na vikundi, walio wengi ni kwa kutokuelewa misingi mikuu ya imani yao ya asili ikiwemo ibada ya Juma Takatifu watu wametiwa mashaka juu ya usahihi wa imani yao.

Tunaona kuwa, sasa hivi tunaishi nyakati za mwisho zilizotabiriwa mvurugiko wa imani unaonekana kwa dhahiri yale waliyoyaacha mitume na mababa wa kanisa yanatiliwa shaka na kubezwa.
Tumechambua kwa undani tatizo la upotoshaji ninakuhamasisha na kukutia moyo kuwa si lazima nawe upotoshwe. Biblia inasema, 'Shika sana ulichonacho' (Ufunuo 3:11). 


Neno la mwisho

Tumekwishaona jinsi msalaba ulivyo mti wa muhimu katika maisha ya wakristo, mengi tumezungumza juu ya mti huo, wengine wamefundisha juu ya kufanya ishara ya msalaba katika vipaji vya nyuso zao. Hiyo yote ni kutaka kuonesha kuwa msalaba siyo kitu cha kawaida.

Kama ni mfuasi wa Kristo unacho cha kujivunia nao ni msalaba wa Yesu....! Waambie watu juu ya mti huo uzaao matunda yake kila siku usiojua kiangazi wala masika hata usiku wala mchanani wa ajabu sana unaookoa siku zote.

Basi wanapoutazama au kuubusu msalaba si kama wanauabudu bali ni kuonesha heshima na upendo wao juu ya mti ambao ni kielelezo cha mti uliotumika kuwakomboa watu wengi.

Kwa maana hiyo tulichojifunza kutoka katika makala hii kuwa wakristo hawaiabudu sanamu ya Yesu ila wanaiheshimu kwa kuwa ndani ya mioyo yao wanajua hakika ya kuwa hawaiabudu ile sanamu bali sanamu ile inabaki kuwa kielelezo tu.


Wao wanamwabudu Mungu tu na Yesu kristo mwana pekee wa mungu na Roho Mtakatifu katika umoja usiogawanyika wenye nafsi tatu.

Wakristo waliojaaliwa kuijua siri ya thamani iliyomo katika msalaba, waoneshe kwa vitendo heshima na upendo wao kwa kuubusu ni tendo la furaha, upendo na uondoe tashwishwi, hofu kwa kuwa tendo hilo ni safi tena ni takatifu na lenye heshima mbele za Mungu. 

MUNGU NA AKUTIE NGUVU ILI USIMAME KATIKA IMANI ILE ILE. 

Makala hii imeandaliwa kwa Msaada wa Bibilia na vitabu mbalimbali vya Kikristo Tanzania.
0716-000447 – 0767-000448
Read More...

Thursday, March 28, 2013

MAUAJI YA KUTISHA MUSOMA KIKONGWE ANYONGWA




 *Wauaji wamfukia shambani kwake baada ya kumuua
 * Wananchi waitupia Serikali na Jeshi la Polisi Lawama
 * Wamkumbuka Kamanda Robert Boaz wataka arudishwe Mara



Ndugu wa Marehemu RoseMary Patrick (72) wakilia na kuomboleza baada ya kumpata akiwa ameuawa kwa kunyongwa kwa kutumia kanga yake na watu wasiojulikana akiwa shambani kwake na kumfukia katikati ya tuta la mihogo katika kijiji cha Bukanga Manispaa ya Musoma, Mkoa wa Mara.

                      
 Askari Polisi PC Regina akifungua kanga shingoni mwa mwili wa marehemu Rosemary Patrick iliyotumika kwa kumnyonga.

Bibi ambaye Jina lake halikupatikana mara moja alibebwa na wasamaria wema baada ya kupoteza fahamu wakati akiomboleza msiba wa ndugu yake Rosemary Patrick aliyeuawa kwa kunyongwa kwa kanga akiwa shambani kwake.
 
 Wananchi wa Kijiji cha Bukanga na maeneo ya jirani waliokusanyika katika shamba la marehemu kuona mauaji ya kinyama ya Bibi Rosemary Patrick (72) alieyeuawa kwa kunyongwa kwa kanga.


 Wananchi wa Kijiji cha Bukanga na maeneo ya jirani waliokusanyika wakiondoka baada ya Polisi kuchukua mwili wa marehemu Bibi Rosemary Patrick (72) alieyeuawa kwa kunyongwa kwa kanga.



 Wananchi wakishirikiana na Jeshi la Polisi kuubeba mwili wa marehemu Rosemary Patrick kutoka sehemu aliyenyongewa na kupelekwa kwenye gari la Polisi kwa ajili ya Kupelekwa Hospitali Kuu ya Mkoa wa mara kwa ajili ya uchunguzi.






 Kaimu Mkuu  wa Upelelezi Wilaya ya Musoma Mjini Justine Shiganza akiuangalia mwili wa marehemu Rosemary Patrick aliyeuawa kwa kunyongwa kwa kanga yake kisha kufukiwa shambani kwake.

Na Thomas Dominick,
Musoma


BIBI mmoja aliyejulikana kwa jina la RoseMary Patrick (72) ameuawa kwa
kunyongwa kwa kutumia kanga yake na watu wasiojulikana akiwa shambani kwake na kumfukia katikati ya tuta la mihogo katika kijiji cha Bukanga Manispaa ya Musoma, Mkoa wa Mara.

Mwandishi wa blog hii alifika katika eneo la tukio na kushuhudia

tukio hilo na kuwatafuta ndugu wa marehemu kisha kufanya nao mahojiano juu ya mauaji hayo ya kutisha.

Tukio hilo ambalo lilitokea Machi 26 saa 12 asubuhi ambapo mume wa
marehamu Msira Masige (76) alisema kuwa mke wake huyo aliamka asubuhi siku ya tukio na  alikwenda kwa ajili ya palizi.

“Mke wangu aliamka asubuhi na kuniaga kisha kuelekea shambani lakini
mpaka inafika majira ya kurudi ambapo kawaida yake yake kurudi saa nne au tano asubuhi, lakini haikuwa hivyo ndipo tulipoamua kwenda shambani kumtafuta bila mafanikio,”alisema Masige.

Alisema kuwa baada ya juhudi za kumtafuta huku na kule walirudisha
juhudi katika maeneo mbalimbali ya shamba hilo ndipo walipobaini kuwa ameuawa na kufukiwa katikati ya tuta la shamba la mihogo.

“Tulirudi tena shambani kwa ajili ya kuendelea kumtafuta na kundi la
wanakijiji wenzetu tukafanikiwa kumpata akiwa amaeuawa na kufukiwa kwenye tuta ndani ya shamba letu,”alisema

Pia mtoto wa marehemu Kulwa Msira (37) alisema kuwa wakati mama yake
huyo akiwa hajulikani alipo  watoto wake walikwenda shambani majira ya saa tatu asubuhi kulima na waliporudi waliulizwa kama wamemuona bibi yao na kujibu kuwa hawakumuona.

“Baada ya watoto wangu kujibu hivyo kwa kuwa kulikuwa na msiba Makoko
tukajua huenda alibadilisha nia na kwenda huko ndipo nilipoanza kupiga simu kila sehemu na kujibiwa kuwa hawajamuaona tukaanza jitihada za kumtafuta huku na kule,”alisema Msira.

Alisema kuwa baada ya kurudi shambani kwake waligundua kuna nyayo za
watu na mtu akiwa ameburuzwa wakafuatilia kisha kukuta mwili wa mama yao mzazi umefukiwa akiwa amesha kufa tayari.

Baada ya askari wa jeshi la polisi kufika eneo la tukio walifukua

mwili wa marehemu kasha kuupakia kwenye gari, ndipo Kaimu kamanda wa Upelelezi Wilaya ya Musoma Mjini Justine Shiganza aliwakusnya wananchi na kuzungumza nao jinsi ya kuweza kushirikiana na Polisi na kufanikisha kuwatia mbaroni wauaji hao.

“Ndugu zangu wa Bukanga poleni sna na msiba huu, lakini lengo la

kuwakusanya hapa ni kutaka kusaidiana jinsi ya kuweza kuwapata wauaji ambao wanaendeleza mauaji katika maeneo yetu kwa kuwa ninyi ndio mnaoishi nao na tunachohitaji wote ni kukomesha matukio haya ya kutisha,”alisema Shiganza.

Alisema kuwa kama kuna mtu ambaye anajua kuna mtu alikuwa na kisasi na
familia hiyo atoe taarifa polisi na kasha yeye mwenyewe aliwapatia namba yake ya simu ya mkononi kwa ajili ya mawasiliano zaidi na kufanikisha kuwakamata wauaji hao.

Baada ya Shiganza kumalizakuongea wananchi walipaza sauti zao na
kulaumu jeshi la Polisi na Serikali kushindwa kuzuia na kukomesha matukio hayo ya kikatili wanayofanyiwa wananchi wa Mkoa huo.

“Matukio haya ya kutisha sasa yamekuwa ya kawaida kwa mkoa wetu hasa
wilaya mbili za Butiama na Musoma Mjini, Serikali na Jeshi la Polisi limekaa kimya kabisa na tumaini wanafurahia kuoana wananchi wao wanauawa ovyo,”alisema Manyonyi Emanueli Mkazi wa kijiji hicho.

Mkazi mwingine wa Kijiji jirani cha Mahare aliyejitambulisha kuwa

Mwenyekiti wa kijiji hicho, John Magesa alisema kuwa mauaji ni tatizo sugu kwa wakazi wa wilaya hizo mbili ambayo inahitaji njia mbadala ya kulipatia ufumbuzi wa kudumu.

“Wauaji wanafanya wanavyopenda tena bila wasiwasi kwa uhuru zaidi
serikali inataka tufanye ulinzi shirikishi nyakati za usiku na wauaji wanafanya matukio yao kuanzia asubuhi, kuna watu wanaonekana wanawinda kwa mbwa na manati lakini ndio wauaji wenyewe hao kinachotakiwa serikali ya wilaya ifanye vikao na serikali za vijiji kuona ni jinsi gani itawalinda wananchi wake,’alisema Magesa.

Wananchi hao hawakusita kusema kuwa Jeshi la polisi kwa sasa halifanyi
kazi yao ipasavyo na matukio hayo yamekuwa mengi baada ya Kamanda wa Polisi Robert Boaz kuhamishiwa Mkoa wa Kilimanjaro ambaye aliunda vikosi kazi vilivyofanya kazi usiku na mchana na kuvisimamia ipasavyo pamoja na kutumia kikamilifu dhana ya Polisi jamii na matukio kama hayo hayakuwepo.

“Hatuji Kamanda wa sasa anafanya kazi gani Mkoani kwetu vikundi vyote
vilivyoundwa kaviua na kama vipo havina nguvu ndio maana wauaji wanapata nafasi ya kuua ndugu zetu Serikali kama inatusikia waturudishie aliyekuwepo mwanzo na huyu apelekwe sehemu nyingine ameshindwa kabisa kulinda maisha ya watu wa Mara,”alisema Kijana Emanuel Rhobi.

Pia waliomba katika matukio kama hayo mbwa wa polisi watumike ili
kubaini wauaji kwani muda mwingine baada ya kuua hufika maeneo hao kushuhudia kama wananchi wema ambapo mbwa hao wataweza kuwabaini walifanya kitendo hicho.

MWISHO.
Read More...

Monday, March 18, 2013

FEDHA ZA KIKWETE ZAWAFIKIA WANANCHI WA WILAYA MPYA YA BUTIAMA





 Mkuu wa Wilaya Mpya ya Butiama Angelina Mabula akifafanua jambo wakati akitoa taarifa ya mafanikio ya Serikali ya awamu ya nne ya Rais JK Kikwete, kuanzia mwaka 2005 hadi 2012.
 Watendaji wa wilaya ya butiama wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya Mpya ya Butiama Angelina Mabula wakati akitoa taarifa ya mafanikio ya Serikali ya awamu ya nne ya Rais JK Kikwete, kuanzia mwaka 2005 hadi 2012.


Na Thomas Dominick,
Butiama

MFUKO wa wajasiliamali unaofadhiliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.Rais Jakaya Kikwete na asasi mbalimbali za kibenki zimeweza kuwakwamua kiuchumi wakazi wa wilaya mpya ya Butiama ambapo jumla ya bilioni 7.370 zilikopeshwa kwa wananchi.


Mafanikio hayo ya Serikili ya awamu ya Nne inayoongozwa na Rais Kikwete kutoka mwaka 2005 hadi 2012 yalitangazwa na Mkuu wa wilaya hiyo ofisini kwake, Angelina Mabula wakati akitoa taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya CCM.

Mabula alisema kuwa katika mfuko wa wajasiriamali Vikundi 4 vya wajasiliamali vilipewa mikopo yenye thamani ya shilingi milioni 180,  Mfuko wa Jamii (TASAF) nao ulitoa shilingi milioni 250 na kukuopeshwa vikundi 32 , Mfuko wa DASIP ulitoa shilingi milioni 400 kwa vikundi 445 vya shamba darasa na benki ya NMB ilitoa shilingi Bilioni 6.64 kwa ajili ya shughuli mbalimbali za kijamiina uchumi kwa wajasiriamali.

“Mfuko wa wajasiriamali wa Rais Kikwete ulitoa fedha kwa vikundi vinne ambavyo ni Mwangaza Saccos ya Buhemba shilingi milioni 80, Imani Bwai (Kiriba) shilingi milioni 31, Mwamucha SACCOS (Mugango) milioni 30 na Ujamaa (Kukirango) milioni 29,”alisema Mabula.

Alisema kuwa TASAF ilitoa fedha kwa vikundi 32 kama ifuatavyo, vikundi vinne ya useremara viliwezeshwa uanzishaji wa karakana na vifaa vyenye thamani ya milioni 38.335, vikundi vya ushonaji na ufumaji viliwezeshwa vyereheni 26 vyenye thamani ya milioni 13.954, vikundi viwili vya akina mama vya usagaji na imewezeshwa mashine mbili za kusaga na kukoboa zenye thamani ya milioni 21.922.

“Vikundi vingine ni kikundi cha walemavu cha ufundi baiskeli kilipata milioni 5.894 na kuanzisha karakana na vifaa vya ufundi baiskeli, Kikundi kimoja cha wazee cha ufugaji ng’ombe 17 kilipatiwa jumla ya milioni. 9.090 zikiwa gharama za ng’ombe 5, ujenzi wa banda, chakula cha nyongeza na tiba Vikundi vya ufugaji kuku 17 vilipatiwa jumla ya milioni 112.078 na Vikundi vya ufugaji mbuzi wa maziwa 3 vilipatiwa jumla ya milioni 20.261,”alifafanua.

Alisema pamoja na mifuko hiyo halmashauri hiyo ipo katika vipaumbele mbalimbali katika kuwakwamua wananchi wake kiuchumi ikiwa pamoja na Kujenga masoko mawili ya kisasa na stendi mbili za mabasi katika Halmashauri ya Wilaya ya Musoma na Butiama.

“Kujenga miradi mikubwa ya umwagiliaji yenye kuongeza fursa za ajira kwa vijana tayari maeneo ya uwekezaji huo yameanishwa na Kukaribisha wawekezaji ili wajenge viwanda,”alisema.

Alisema kuwa zoezi la upimaji liko katika hatua nzuri ili kuweka mji katika utaratibu wa mipango mji. Mara taratibu zote zitakapokamilika matangazo yatatolewa kwenye vyo vya habari ili kila mhitaji apate kiwanja bila usumufu.

MWISHO
Read More...