Friday, September 20, 2013

MWENGE UMEFUNGUA, UMEZINDUA NA KUKAGUA, YAWEKA JIWE LA MSINGI MIRADI 11 YENYE THAMANI YA TSHS MILIONI 672.922 WIALAYA YA NANYUMBU MKOA WA MTWARA






 MKUU WA WILAYA YA NANYUMBU FESTO KISWAGA AKIMSIKILIZA MMOJA WA KIONGOZI WA WILAYA HIYO KATIKA SHEREHE ZA UPOKEAJI WA MWENGE KATIKA KIJIJI CHA ULANGA WILAYANI HUMO UKITOKEA WILAYA YA MASASI.


 WANANCHI WA WILAYA YA NANYUMBU MKOA WA MTWARA WAKIWA KATIKA SHANGWE KUBWA KWA AJILI YA KUUPOKEA MWENGE WA UHURU UNAOTOKEA WILAYA YA MASASI.

 WANANCHI WA WA WILAYA YA NANYUMBU WAKIWA WAMEFURIKA KATIKA KIJIJI CHA NANYUMBU KUUPOKEA MWENGE WA UHURU ULIOTOKEA WILAYA YA MASASI.


 MKUU WA WILAYA YA NANYUMBU FESTO KISWAGA AKIWA KATIKA VIWANJA VYA MAKABIDHIANO YA MWENGE WA UHURU KATIKA KIJIJI CHA ULANGA WILAYANI HUMO.
 MWENGE WA UHURU UKIWASIRI KATIKA KIJIJI CHA ULANGA MPAKANI MWA MASASI NA NANYUMBU KWA AJILI YA KUANZA MBIO ZAKE WILAYA YA NANYUMBU.

 MKUU WA WILAYA YA NANYUMBU FESTO KISWAGA AKISALIMIA NA MMOJA WA WAKIMBIZA MWENGE BAADA YA KUWAPOKEA WAKITOKEA WILAYA YA MASASI
  MKUU WA WILAYA YA NANYUMBU FESTO KISWAGA AKIKUMBATIANA NA MMOJA WA WAKIMBIZA MWENGE WA KITAIFA KATIKA KIJIJI CHA ULANGA BAADA YA KUKABIDHIWA KUTOKEA WILAYA YA MASASI
  MKUU WA WILAYA YA NANYUMBU FESTO KISWAGA AKIWA NA KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE JUMA ALI SIMAI WAKIMSIKILIZA MKUU WA WILAYA YA MASASI
 MKUU WA WILAYA YA MASASI FATUMA AKIWA AMEUSHIKA MWENGE WA UHURU TAYARI KUMKABIDHI MKUU WA WILAYA YA NANYUMBU FESTO KISWAGA.
 MKUU WA WILAYA YA MASASI FATUMA AKIZUNGUMZA JAMBO FULANI KABLA YA KUMKABIDHI MWENGE WA UHURU MKUU WA WILAYA YA NANYUMBU FESTO KISWAGA.
 MKUU WA WILAYA YA NANYUMBU FESTO KISWAGA AKIPOKEA MWENGE WA UHURU KUTOKA KWA MKUU WA WILAYA YA MASASI FATUMA
 MKUU WA WILAYA YA NANYUMBU FESTO KISWAGA AKISEMA JAMBO BAADA YA KUPOKEA MWENGE WA UHURU TOKA KWA MKUU WA WILAYA YA MASASI FARIDA MGOMI ALIYEINAMIA CHINI

 MWENGE WA UHURU UKIWA UMEANZA MBIO ZAKE WILAYA YA NANYUMBU BAADA YA KUTOKA WILAYA YA MASASI
 MKUU WA WILAYA YA NANYUMBU FESTO KISWAGA AKIMSIKILIZA MMOJA WA WAKIMBIZA MWENGE KITAIFA KATIKA UFUNGUZI WA BARABARA YA NANDETE CHIVIRIKITI.
 KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE JUMA ALI SIMAI AKIFUNGUA GHALA LA KUHIFADHIA MAZO KATIKA KIJIJI CHA MCHANGANI A WILAYA YA NANYUMBU MKOA WA MTWARA.

 KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE JUMA ALI SIMAI AKIKRIKI KWENYE KOMPUTA WAKATI AKIFUNGUA KITUO CHA WALIMU KATA YA MIKANGAULA.

 MKUU WA WILAYA YA NANYUMBU FESTO KISWAGA AKIPANDA MTI KWENYE CHANZO CHA MAJI KATIKA KIJIJI CHA NANGOMBA KWENYE BUSTANI YA VIJANA YA MBOGAMBOGA
 KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE JUMA ALI SIMAI AKIFUNGUA MAJI WAKATI AKIZINDUA MRADI WA MAJI SAFI NA SALAMA KATIKA KIJIJI CHA NDWIKA WILAYANI NANYUMBU

 WANANCHI WA WILAYA YA TUNDURU MKOA WA RUVUMA WAKICHEZA KATIKA MAKABIDHIANO YA MWENGE WA UHURU AMBAO ULIKUWA UNATOKA MKOA WA MTWARA NA KUINGIA MKOA WA RUVUMA KATIKA KIJIJI CHA SAUTI MOJA KILICHOPO MPAKANI MWA WILAYA YA NANYUMBU NA TUNDURU
 MKUU WA WILAYA YA NANYUMBU FESTO KISWAGA AKIMKABIDHI MKUU WA MKOA WA MTWARA KANALI JOSEPH SIMBAKALI KABLA YA KUUKABIBHI KWA MKUU WA MKOA WA RUVUMA SAIDI MWAMBUNGU KWA AJILI YA KUANZA MBIO ZAKE KATIKA WILAYA YA TUNDURU MKOA WA RUVUMA.
MKUU WA MKOA WA MTWARA JOSEPH SIMBAKALI AKIMKABIDHI MWENGE WA UHURU MKUU WA MKOA WA RUVUMA SAID MWAMBUNGU.  


Na Thomas Dominick,
Nanyumbu

MIRADI 11 yenye thamani ya Milioni 672.922 imefungua na kuweka jiwe la msingi, Kukagua na kuzindua na Mwenge wa Uhuru katika Wilaya ya Nanyumbu, Mkoa wa Mtwara.

Akisoma risala ya utii ya wananchi wa wilaya hiyo kwa Rais wa Jakaya Kikwete, mbele ya kiongozi wa mbio za mwenge Juma Ali Simai Mkuu wa wilaya hiyo Festo Kiswaga alisema kuwa miradi hiyo inatoka katika sekta ya miundombinu, elimu ya msingi na sekondari, kilimo, maji, Nishati, ujasiriamali na utawala bora.

“Miradi hiyo iliyotekelezwa ilipata fedha kutoka katika vyanzo mbalimbali ambapo nguvu za wananchi zilikuwa Tshs Milioni 268.238, Serikali kuu tshs. Milioni 325.026, Halmashauri ya wilaya tshs milioni 62.113 na wahisani tshs. Milioni 17.544,”alisema.

Alisema kuwa katika mgawanyo sawa wa rasilimali wilya hiyo inajitahidi kuzingatia uwiano katika kutoa huduma mbalimbali za kijamii na za kiuchumi katika kata 14 kupitia miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwenye ngazi hiyo.

“Aidha tumekuwa makini kuhakikisha kwamba watumishi wanaopangiwa wilayani kwetu wanagawanywa kwa uwiano unaozingatia mahitaji kwenye maeneo husika kama vile walimu wa shule za msingi na sekondari, wataalam wa afya, watendaji vijiji na kata,”alisema Kiswaga.

Alisema kuwa pamoja na mafanikioya wilaya hiyo pia kuna changamoto zinazowakabili ambazo zinahitaji msukumo na ufunbuzi wa kitaifa, ambapo moja ya changamoto hizo ni tatizo la upatikanaji wa maji safi na salam.

“Kwa sasa asilimia 28.7 tu ya wananchi wanapata maji safi na salama pia tuna upungufu wa watumishi wenye taaluma mbalimbali aidha wilaya ina uhaba wa vyombo vya usafiri hususani magari kwa ajili ya matumizi ya ofisi kwenye idara mbalimbali,”alisema.

Mwenge huo ulipokelewa katika Kijiji cha Ulanga kukimbizwa kilometa 124 na kukabidhiwa katika kijiji cha shauri moja mpakani mwa wilaya hiyo na mkoa wa ruvuma.

Miradi iliyopitiwa na mwenge huo ni ujenzi wa barabara kutoka Nandete hadi Chivirikiti yenye urefu wa Kilometa 7, madarasa mawili katika shule ya sekondari maratani, ghala la kuhifadhia mazao kijiji cha mchangani na kituo cha uendelezaji walimu (TRC).

Mingine ni upandaji miti kwenye chanzo cha maji nangomba, kilimo cha bustani za mbogamboga kinachoendeshwa na vijana wa nangomba, maji ya bomba ndwika, kituo cha mafuta cha Kinjikitile, banda la mama wajasiriamali, Afya, ukimwi, polisi na dawa za kulevya na banda la TAKUKURU yote ya mjini mangaka.


MWISHO

Read More...

Saturday, September 14, 2013

TASAF YAMWAGA BILION 1.7 KATIKA MIRADI MBALIMBALI WILAYA YA NANYUMBU MKOA WA MTWARA.






 Vijana Kikundi cha sanaa cha mjini mwema wakionesha umahiri wao mbele ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais mahusiano na Uratibu Stevin Wasira aliyefika katika kijiji hicho kwa ajili ya kukagua mradi wa miti kwa ajili ya kulinda vyanzo vya maji
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais mahusiano na Uratibu Stevin Wasira akisalimiana na viongozi wa kijiji cha Michiga ndani ya wilaya ya Nanyumbu.
 Wananchi wa Msinyasi wakimsikiliza Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais mahusiano na Uratibu Stevin Wasira(hayupo pichani) baada ya kukagua mradi wa barabara iliyounganisha kati ya kijiji cha magomeni na msinyasi yenye urefu wa KM 9.8
 Moja ya ufadhili wa TASAF wa umeme wa jua katika shule ya sekondari ya Sengenya
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mahusiano na Uratibu Stevin Wasira akisikiliza risala ya kikundi cha wajane na wagane wa kikundi cha ufugaji kuku katika kijiji cha ngalinje.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais mahusiano na Uratibu Stevin Wasiraakimsikiliza mjane Hadija Mrope kabla ya kukagua mradi wa ufugaji wa kuku uliofadhiliwa na TASAF katika kijiji cha Ngalinje Wilaya ya Nanyumbu Mkoa wa Mtwara.
 Watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya nanyumbu wakimsilikiza Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais mahusiano na Uratibu Stevin Wasira kwenye ukumbi wa mikutano wa mkuu wa wilaya.
 Mkuu wa Wilaya ya Nanyumbu Mkoa wa Mtwara Festo Kiswaga akimkaribisha Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais mahusiano na Uratibu Stevin Wasira alipowasili wilayani humo kwa ajili ya ziara ya siku moja kukagua na kujionea shughuli za maendeleo ya wananchi kwa ufadhili wa TASAF.



Na Thomas Dominick,
Nanyumbu

Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF)  awamu ya pili umetoa jumla ya Tshs Bilioni  1.7 kwa ajili ya kufadhili miradi 85 katika vijiji mbalimbali vya Wilaya ya Nanyumbu, Mkoa wa Mtwara.

Akitoa taarifa fupi ya maendeleo ya wilaya hiyo kwa Waziri wa Nchi  ofisi ya Rais Mahusiano na Uratibu Stevin Wasira aliyekuwa katika ziara ya kukagua miradi iliyofadhiliwa na TASAF Mkuu wa wilaya Festo Kiswaga alisema kuwa TASAF imesaidia kuinua maisha ya wananchi ya wilaya hiyo katika nyanja mbalimbali.

Kiswaga alisema kuwa jumla ya miradi 75 imekamilika na miradi ambayo ipo katika hatua ya utekelezaji ni miradi 10 iliyoanza Julai mwaka huu na pia kuna miradi 14 inayosubiri fedha kutoka TASAF.

“Miradi iliyokuwa katika hatua ya utekelezaji ni miradi sita ya ujenzi wa barabara, miradi mitatu ya uhifadhi wa mazingira na mradi mmoja wa hifadhi msitu shirikishi,”alisema Kiswaga.

Pia alisema kuwa wilaya hiyo inakabiliwa na upungufu mkubwa wa vyumba vya madarasa, nyumbza za walimu, zahanati na mabweni kwa shule za sekondari.

“Hivyo watoto wanasoma katika mazingira magumu na pia walimu kufundisha katika mazingira magumu na duni hii inachangia kushuka kwa elimu,” alisema.

Mkuu huyo wa wilaya alitumia fursa hiyo kuiomba TASAF ione uwezekano wa kuiwezesha Halmashauri hiyo kutatua tatizo hilo kwani serikali inajitahidi kuwashirikisha wananchi katika mipango mbalimbali ya maendeleo.

Naye Waziri Wasira aliwaomba wananchi kutumia fursa zinazotolewa na serikali ili kuweza kujiletea maendeleo yao wenyewe na kujikwamua kutoka katika umasikini uliokithiri katika jamii.

“Mipango ya TASAF ni endelevu ili kuwainua wananchi wetu kutoka katika umasikini na kuishi maisha  mazuri pia tunawashauri wataalamu wetu kuwa karibu na wananchi kuwapatia mafunzo bora ya kilimo, ufugaji na uzalishaji mali,”alisema Wasira  

Wasira aliwaomba viongozi wa TASAF alioambatana katika ziara hiyo wanatakiwa kujifunza na kuona matatizo yanayowakabili wananchi na kufikiria zaidi familia maskini.

Miradi aliyotembelea ni pamoja na kikundi cha ufugaji kuku cha wajane na wagane kilichopo kijiji cha Ngalinje, ujenzi wa barabara kuunganisha kijiji cha magomeni na msinyasi na barabara yenye urefu wa Km 4 inayounganisha kitongoji cha Mikangaula na kijiji cha Nakopi.

Miradi mingine ni ujenzi wa masijala ya kutoa hati miliki katika kijiji cha michiga na  mradi wa kupanda miti kwenye vyanzo vya maji katika kijiji cha Nangomba ambapo kwa sasa kuna vitalu takribani 20 na wanatarajia kupanda miti hiyo mwezi Desemba mwaka huu.


Read More...