Sunday, April 21, 2013

PSPF YAWAJENGEA UELEWA WA MFUKO HUO WANACHUO WA CHUO CHA UALIMU BUNDA HIVI KARIBUNI



 *Wanachuo hao wataka umri wa kustaafu ushuke hadi miaka 40
*PSPF yajenga nyumba kwa ajili ya kuwakopesha wanachama wao
*Vijana wapendelewa zaidi na mfuko huo


Afisa Mfawidhi wa Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma Sudi Hamza akiandika fomula ya kupata mafao kwa wanachuo wa chuo cha ualimu Bunda wanaotarajia kuanza mitihani yao mei 6 mwaka huu na kupata ajira ya Serikali
 Wanachuo wa chuo cha Ualimu Bunda wakimsikiliza kwa makini Afisa Mfawidhi wa Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma Sudi Hamza katika semina ya siku moja chuoni hapo.
 Afisa Mfawidhi wa Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma Sudi Hamza akiwaelezea wanachuo wa chuo cha Bunda umuhimu wa kujiunga na mfuko wa pensheni kwa watumishi wa umma na mafao ambayo wanaweza kupata wakiwa wananchama wa mfuko huo.
 Wanachuo wa Chuo cha Ualimu Bunda wakipata soda baada ya kumalizikia semina ya Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma PSPF iliyofanyika chuoni hapo ili kuwajengea uwezo wa kuufahamu vizuri mfuko huo..


 Wanachuo wakisoma vipeperushi vya Mfuko wa Pensheni kwa watumishi wa Umma (PSPF) katika semina ya siku moja iliyofanyika chuoni hapo.


 Afisa Mfawidhi wa Mfuko wa Pensheni kwa watumishi wa Umma (PSPF) Mkoa wa Mara Sudi Hamza akitoa formula  kwa wanachuo wa Chuo cha Ualimu Bunda jinsi ya kupata mafao yako ya uzee baada ya kustaafu.
 Wanachuo wa chuo cha Ualimu bunda wakimsikiliza Afisa Mfawidhi wa PSPF Sudi Hamza wakati wa semina ya siku moja kwa ajili ya kuwajengea uwezo na uelewa wa mfuko huo.

Na Thomas Dominick,
Bunda

MFUKO wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF) umewajengea uwezo na ufahamu wa mfuko huo wa Pensheni wanachuo wa Chuo cha Ualimu Bunda kilichopo wilaya ya Bunda Mkoani Mara wanaotarajia kuajiriwa na Serikali mwaka huu.

Akitoa semina ya siku moja chuoni hapo Afisa Mfawidhi wa PSPF  Mkoa wa huo, Sudi Hamza aliwataka wanachuo hao wanaotarajia kuanza mitihani ya mwisho mei 6 mwaka huu kuwa makini na mifuko hiyo pindi watakapoajiri na Serikali.

“Nimekuja chuoni hapa kwa ajili ya kufanya semina na ninyi ili kuwapatia ufahamu wa na kuwaongezea uwezo wa kuutambua vizuri mfuko wa PSPF na kujua faida ya kujiunga nao kwani ndio unaotoa faida kubwa kwa wanachama wake,”alisema Hamza.

Baada ya Hamza kuwasilisha mada juu ya mfuko huo wanachuo hao walipewa nafasi ya kuuliza maswali na mapendekezo mbalimbali ambayo yangeweza kuwajenga zaidi.

Ambapo mwanchuo aliyejulikana kwa jina la Kinguye Wambura aliiomba PSPF kwa kushirikiana na Serikali kujadili kwa kina juu ya umri wa kustaafu kwa watumishi kutoka miaka 55 ya hiari na 60 ya lazima hadi kufikia 40 hadi 45.

“Hii hali ya kusubiria hadi miaka 55 na 60 ni ni uonevu kwa watumishi kwani hadi kufikia umri huo mtumishi anakuwa hana nguvu ya kufanya biashara na akili inakuwa imechoka haitamnufaisha fedha hiyo kwani akili inakuwa imechoka hivyo Serikali ipunguze miaka hadi 40 na 45 ya lazima,” alisema Wambura.

Naye mwanachuo aliyejitambulisha kwa jina la Agnes Ezekiel alimuuliza Afisa huyo kuwa kama kuna uwezo wa kujiunga na mifuko zaidi ya mmoja kwa ajili ya kupata mafao mengi pindi atakapostaafu.

Hamza alimjibu  kuwa hiyo haiwezekani kujiunga na mfuko zaidi ya mmoja labda ajiunge na Mfuko wa Hiari uliopo chini ya PSPF ambapo atalipwa mafao yake baada ya kuwekeza ambapo fedha hiyo isipungue sh. 10,000/= kwa mwezi.

Alisema kuwa pia PSPF inatoa mafao ya Elimu ambapo kama mwanachama anataka kwenda kusoma yeye ama motto wake unampatia fedha hizo kwa ajili ya kulipia ada, aliongeza kuwa PSPF inatoa mafao ya ujasiriamali kwa mwanachama ambaye anataka kuanzisha biashara.

Pia alisema kuwa PSPF inajenga nyumba sehemu mbalimbali kwa ajili ya kuwakopesha wanachama wake waliotimiza miaka mitano ili kuwakwamua kimaisha ambapo mwanachama atatakiwa kulipa ndani ya miaka 25.

“Kutokana na kujua ugumu wa maisha tumeamua kujikita katika kujenga nyumba bora za kisasa kwa ajili ya kuwakopesha wanachama wetu ambazo watalipa ndani ya mika 25 na sharti kuu lazima atomize miaka mitano kazini,”alisema.

Hamza aliwatoa wasiwasi wanachuo kuwa serikali imeweka ofisi kila mkoa kwa ajili ya kupunguza usumbufu kwa wanachama wao kusafiri kufuatilia mafao yao Makao Makuu Dar es Salaam na kufuata ushauri na maelekezo mbalimbali.

Kwa sasa mtumishi akiwa na shida hana haja ya kwenda Makao Makuu ya PSPF anachotakiwa ni kwenda makao makuu ya Mkoa kwani kila mkoa kuna ofisi yetu kwa ajili ya ushauri na kama una tatizo linamalizikia hapo tena bila usumbufu wowote,”alisema.

PSPF imejipanga kutoa semina kwa wanachuo mbalimbali ambayo wanatarajia kuingia katika soko la ajira hasa wanaoajiriwa na serikali ili kuweza kupata mafao bora pindi wakapofikia umri wa kustaafu.








0 comments:

Post a Comment