Saturday, August 17, 2013

KIAMA CHATANGAZWA KWA WATENDAJI KATA NA VIJIJI, WAKULIMA NA WACHOMA MKAA WA WILAYA YA BUTIAMA MKOA WA MARA.







 Hii ni sanamu ya baba wa Taifa iliyowekwa nje ya ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama.
 Mkuu wa Wilaya ya Butiama akizungumza jambo fulani na waandishi wa habari ofisini kwake.

Na Thomas Dominick,

Butiama



WATENDAJI wa Kata na Vijiji Wilaya ya Butiama, Mkoa wa Mara kukiona cha moto endapo wataendelea kuwaruhusu wananchi wao kulima maeneo oevu na wanaoendelea kukata miti ovyo na kuharibu mazingira ambayo itasababisha jangwa.



Kauli hiyoi ilitolewa na Mkuu wa Wilaya hiyo, Angeline Mabula wakati akifungua kikao ca Ushauri cha Wilaya (DCC) kwa kilichoitishwa kwa ajili ya kujadili ugawaji wa raslimali na madeni ya Halmashauri ya Musoma kutokana na kuigawa Halmashauri hiyo katika wilaya mbili ya Butiama na Musoma ambapo inapigiwa debe iitwe wilaya ya Nyanja.



Mabula alisema kuwa wananchi wa wilaya ya Butiama wamekuwa wakilima maeneo oevu na kusababisha ukame ambao unatishia maisha ya viumbe hai pamoja na binadamu wanaoishi kuzunguka maeneo hayo.



“Nitafanya ziara kupitia sehemu mbalimbali kukagua maeneo oevu na nikikuta wananchi wanalima sitahangaika na mkulima huyo bali badala yake nitaanguka na mtendaji wa eneo hilo kwani atakuwa ameshindwa kutekeleza sheria za mazingira,”alisema Mabula.



Pia alisema kuwa wilaya hiyo inaongoza kwa kukata miti na kuchoma mkaa ambapo pia aliahidi kufanya oparesheni hivi karibuni ya kuwakamata wauza mkaa wanaotokea wilaya hiyo na akihojiwa na kusema kata anayotoka atachukuliwa hatua yeye na mtendaji wa eneo hilo ambapo watapelekwa kwenye vyombo vya sheria sambamba na kuwashitaki.



Baada ya tamko la Mkuu wa wilaya wajumbe waliokuwepo katika mkutano huo waliguna kwa pamoja ndipo alipoamua kukazia usemi wake, “ Nyie mgune tu lakini nitakapopita maeneo yenu na kufanya opresheni hiyo ndipo mtakapojua nini nakimaanisha sitanii kwa hili,”alisema.



Ndipo alipomuagiza Mkurugenzi wa wilaya hiyo Fidelica Myovela kuhakikisha anatenga maeneo maalumu kwa ajili ya kukata miti na kuchoma mkaa na sio kila eneo lenye miti litumike kwa shughuli hiyo. 

Mwisho.

0 comments:

Post a Comment