Thursday, August 15, 2013

MKUU WA WILAYA YA BUTIAMA MKOA WA MARA AWATIMUA VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA KWENYE KIKAO CHA USHAURI WA WILAYA (DCC)







 MKUU WA WILAYA YA BUTIAMA ANGELINA MABULA AKIWA OFISINI KWAKE (PICHA KUTOKA MAKTABA YA BLOG)


Na Thomas Dominick,
Musoma.

MKUU wa Wilaya ya Butiama Mkoa wa Mara Angelina Mabula amewafukuza viongozi wa vyama vya siasa kwenye kikao cha Ushauri cha Wilaya hiyo (DCC) baada ya wajumbe kuibua vurugu kubwa na kuwataka viongozi hao ambao vyama vyao havipo wilayani humo kuondolewa kwenye kikao hicho.

Kikao hicho kilichoanza kwa wajumbe kutoka kwenye baadhi ya vyama vya upinzani kumuomba Mkurugenzi Fidelica Myovela kuwaondoa viongozi hao ambao aliwapa mialiko kinyemelea wakati hawafanyi kazi katika wilaya hiyo.

“Wakulaumiwa ni wewe Mkurugenzi kutokana na utaratibu wako mbovu uliotumia kuwaalika viongozi ambao sio wa Butiama na hawana ofisi katika wilaya yetu hawa wote ni viongozi wa Manispaa ya Musoma,”alisema    Richard Choge Katibu wa Chadema wilaya hiyo.

Baada ya shutuma hizo kwa Mkurugenzi ndipo Mkuu wa Wilaya kabla ya kufungua kikao hicho alitoa tamko zito  la kuwataka kuondoka ndani ya ukumbi huo viongozi hao ambao hawana ofisi wilayani humo.

“Sitaki vurugu kwenye kikao change hivyo nawaomba wale ambao hawausiki na wilaya yetu watoke nje mara moja kabla sijawatoa kwa nguvu sipendi tuanze vibaya,”alisema Mabula.

Baada ya tamku hilo Kamanda wa Polisi wa Wilaya hiyo Audax Majaliwa aliingilia kati na kuwatoa nje huku akiomba askari kwa ajili ya ulinzi ambapo baada ya dakika kadhaa askari waliongezeka na kuzunguka ukumbi huo na hali kurudi kuwa shwari na kuendelea na kikao.

Vyama ambavyo viongozi wake walifukuzwa ni pamoja na UDP, NLD, NCCR Mageuzi, TADEA,ADCDEMOKRASIA MAKINI na SAU ambavyo vyote havia ofisi ndani ya wilaya hiyo.

Akifungua kikao hicho Mabula aliwataka wajumbe kutumia nafasi hiyo kutoa ushauri bora ambao utakwenda kwenye kikao cha Ushauri wa Mkoa (RCC) ili kupata Baraka ama kuhalalishwa na kuwa taarifa kamili ya wilaya na mkoa kwa jumla.

Katika taarifa yake alisema kuwa wilaya hiyo inatakiwa kugawanywa kwa rasilimali na madeni ya halmashauri ya Musoma ambayo itavunjwa rasmi Augosti 20 mwaka huu na kuwaomba kuwa usikivu wao katika kupitia taarifa mara itakapowasilishwa ili iwe manufaa kwa wana butiama.

“Ndugu wajumbe ni imani yangu kuwa mtatumia nafasi hii vizuri katika kufikia ushauri wenye tija, mtakuwa na nafasi nzuri ya kutafakari kwa kina kwa manufaa ya wote aidha mtatoa ushauri wenye tija ukizingatia kuwa pamoja na halmashauri kugawanywa bado halmashauri zote mbili zitaendelea kuwa chini ya wilaya ya Butiama,”alisema.

Aliongeza kuwa lengo la kugawa halmashauri hiyo ni kusogeza huduma kwa wananchi  pia yawezekana kuwa njia ya baadaye kupata wilaya inayojitegemea mwenendo mzimahuo ni kwa ajili ya kuijenga na kuiimarisha wilaya katika mustakabali wa kumuenzi muasisi wa Taifa hilo Hayati Mwl. Julius Nyerere ambaye amepewa heshima kubwa.   

MWISHO.

0 comments:

Post a Comment