Wednesday, February 13, 2013

MWOSHA MAGARI AANGUSHA GARI LA MTEJA WAKE

 Gari aina ya Ardeo D 4 Toyota lenye namba ya usajili T 904 BET ikiwa chini ya daraja lililopo njia ya kuelekea Majita Road baada ya dereva wa gari hilo Himis Mchongole  kushindwa kulithibiti na kuingia Darajani karibu na makazi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.


 Askari wa Usalama Barabarani akiwa katika shughuli ya kupima eneo la ajali ya gari lenye namba T 904 BET lililopata ajali Leo asubuhi
 Kijana Hamis Mchongole ambaye alikuwa anaendesha gari lililopata ajali akiwa katika gari la Polisi baada ya kuokolewa kutoka ndani ya gari hiyo.
Askari wa Usalama barabarani akiendelea na upimaji wa ajali hiyo.




Na Thomas Dominick,
Musoma

Gari lenye namba T 904 BET lililokuwa likiendeshwa na kijana Hamis Mchongole lilianguka na kuharibika vibaya baada ya dereva huyo kushindwa kulimudu na kuingia darajani katika barabara ya Majita, Manispaa ya Musoma, Mkoa wa Mara.

Tukio hilo limetokea Leo asubuhi katika daraja linalotenganisha kati ya mtaa wa mukendo na Mwisenge maarufu Majita Road, inadaiwa kuwa dereva wa aliyekuwa anaendesha gari hilo ni mwosha magari wa eneo la Uwanja wa Ndege Mjini hapo.

Mwandishi wa Blog hii alifika katika eneo la tukio na kudodosa kisa cha gari hiyo kuingia darajani humo ambapo baadhi ya mashuhuda walisema kuwa kijana huyo alikuwa anaendesha gari hilo kwa mwendo wa kasi.

Inadaiwa kuwa gari hiyo ilipeleka kwa mwosha magari kwa ajili ya ya kufanyiwa usafi lakini aliacha funguo za gari, jina la Mmiliki wa gari hilo halikuweza kupatikana mara moja ili kuelezea ni jinsi gani gari lake liliendeshwa na mwosha magari huyo na kama alikuwa amemuagiza.

MWISHO
Read More...

Tuesday, February 12, 2013

MCHUNGAJI AKANUSHA VIKALI TAARIFA ZILIZOTOLEWA NA RADIO FREE AFRICA



Baadhi ya Waandishi wa habari wa Mkoa wa Mara wakiwa katika chumba cha mchungaji Daudi Makoye kwa ajili ya kwenda kusikilza wito walioitiwa na mchungaji huyo.

MWENYEKITI wa Kanisa la Waadventista wasabato Jimbo la Mara na Ukerewe (Mara Conference), Daudi Makoye amekanusha vikali mbele ya waandishi wa habari taarifa  iliyotolewa na Radio  Free Africa kuwa Mchungaji wa Kanisa hilo la Ukerewe, Emmanuel Tarara kuwa amebaka mtoto mwenye umri wa miaka minane na kwamba huyo si mchungaji wa kanisa hilo.


 
Na Thomas Dominick,
Musoma.

MWENYEKITI wa Kanisa la Waadventista wasabato Jimbo la Mara na Ukerewe (Mara Conference), Daudi Makoye amekanusha vikali taarifa  iliyotolewa na Radio  Free Africa kuwa Mchungaji wa Kanisa la Waadvetista wa Sabato la Ukerewe, Emmanuel Tarara kuwa amebaka mtoto mwenye umri wa miaka minane na kwamba huyo si mchungaji wa kanisa hilo.

Sambamba na kumtaka mtangazaji wa redio hiyo Jovinta Kaijage kukanusha mara moja na kuomba radhi kwa kanisa hilo na watanzania kwa ujumla la sivyo watamchukulia hatua yeye na chombo chake.

Akizungumza na waandishi wa habari katika Kanisa la waadventisa wa sabato la Kamunyonge,  Mchungaji Makoye  alisema kuwa taarifa hiyo iliyotangazwa juzi katika kipindi chake cha “Matukio” kinachotangazwa kuanzia saa moja ya asubuhi, ilitangazwa na mwandishi wake Jovinta Kaijage kutoka Ukerewe.


"Tunapenda kukanusha vikali taarifa hii kwa sababu hauna ukweli wowote Kanisa la Waadventista Wasabato kwa sasa ina wachungaji watatu katika wilaya ya Ukerewe.”alisema Mchungaji Makoye.

Aliwataja wachungaji wa Ukerewe ni pamoja na Mchungaji Elifamili Kashanga anayesimamia mtaa wa Mrutunguru, Mchungaji Kapete Mafuru anayesimamia mtaa wa Ilangara.

Mitaa mingine inasimamiwa na Mchungaji Zefa Ayugi anayesimamia mtaa wa Buhima na mtaa wa Nansio unasimamiwa na Mzee wa kanisa ndugu Staford Maiga anayekaimu nafasi ya mchungaji Daniel Muhono aliyehamia Mtaa wa Buturi hadi atakapopelekwa  mchungaji mwingine. 

Alisema kuwa kutokana na taarifa hizo waliwasiliana na Mzee wa kanisa, Staford Maiga wa Nansio ambaye walizungumza nae kwa simu juu ya jina hilo na kuthibitisha kuwa  Emmanuel Tarara hata si mshiriki wa kanisa hilo.

Aidha amewaomba  waandishi wa habari na hasa wa chombo kilihusika (RFA) kutoa taarifa sahihi iliyofanyiwa uchunguzi  na kuhakikishwa kisha kuutangaza kwa wananchi. 

“Waandishi wa habari ni watu waliiopewa  dhamana ya kuelemisha na kudumisha amani ya umma ya watanzania na kokote na kwamba  ni taarifa za uhakika tua nizo zinazosikika, hivyo  si vizuri kutoa taarifa isiyo sahihi na yenye malengo mbaya kwa  hisia za watu na inayoweza kuleta mfarakano na fitina katika jamii,”alisema.

Pia taarifa isitolewe ambayo inaweza kuleta picha mbaya au kupaka matope dhehebu na kuharibia sifa ya kanisa hivyo pamoja amemtaka Mwandishi huyo aombe radhi kwa jumuia ya kanisa la Waadventista Wasabato na watanzania wengine waliosikiliza habari hiyo  kurekebisha taarifa hiyo haraka.

MWISHO. 
Read More...

Thursday, February 7, 2013

MAUAJI MENGINE BUTIAMA, WANAJESHI WAZUIA MAAFA








 Gari ya Jeshi la Polisi likiwa linatokea eneo la tukio la mauaji kijiji cha Etaro ambapo walichukua mwili wa marehemu Magere Masatu na kuupeleka Hospitali ya Mkoa wa Mara.
 Askari wa kutuliza ghasia wa Mkoa wa Mara wakiwa katika eneo la tukio kuzuia ghasia kutoka kwa waendesha pikipiki na wananchi wa kijiji cha Etaro wilaya ya Butiama
 Wananchi wa Kijiji cha Etaro wakiangalia nyumba ya Magee Saganda iliyochomwa moto baada ya mtoto wake Koti Magee kudaiwa kuhusika katika mauaji ya mwendesha pikipiki.
 Baiskeli zikiwa zimeungua ndani ya nyumba ya mtuhumiwa wa mauaji ya kijana Magere Masatu.
 wananchi wa Etaro wakishangaa tukio la uchomaji wa moto nyumba ya kijana anayetuhumiwa tukio la mauaji.


Na Thomas Dominick,
Butiama

MAUAJI ya kutisha bado yanaendelea kutokea katika Wilaya ya Butiama, Mkoa wa Mara baada ya kijana mmoja aliyetambulika kwa jina la Magere Masatu Mkazi wa Mtaa wa Nyakato, Wilaya ya Musoma kuuawa kasha kutupwa kwenye Mto wenye maji.

Katika tukio hilo Wanajeshi waliingilia kati na walifanikiwa kudhibiti maafa zaidi baada ya nyumba moja ya mtuhumiwa wa mauaji hayo kuchoma moto na kuteketeza kila kitu.

Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo wanadai kuwa tukio hilo lilitokea tarehe Februari 4 mwaka huu katika kijiji cha Etaro wilayani humo, ambapo walisema kuwa siku ya tukio marehemu aligongana na pikipiki na mwenzake ambaye akufahamika jina lake.

Walisema kuwa baada ya kugongana marehemu aliamua kumlipa fedha aliyegongana naye lakini balozi wa eneo la tukio alipelekewa pikipiki ya marehemu kwa ajili ya kuihifadhi.

“Baada ya tukio kweli pikipiki ilichukuliwa na kupelekwa kwa balozi wakati wanakwenda kuna vijana wawili walikuwa wakifuatilia kwa nyuma, na baada ya hapo marehemu hakuonekana tena hadi jana alipoonekana amekufa na yupo ndani ya mto,”alisema shuhuda aliyekataa kutaja jina lake.

Baada ya waendesha pikipiki wa Wilaya ya Musoma kupata taarifa kwa kuuwa kwa mwenzao walikwenda na kuvamia kijiji hicho kwa kuwapiga baadhi ya wananchi na balozi ambaye alikuwa amehifadhi pikipiki hiyo kisha kumtaja mmoja wa wauaji hao kuwa ni Koti Magee mkazi wa kijiji hicho.

Waendesha pikipiki hao walikwenda hadi kwa mtuhumiwa huyo na walimkuta lakini alifanikiwa kuwatoroka kisha kukimbilia ziwani na kujitosa kwenye maji kuogelea ikiwa ndio pona yake.

Baada ya kumkosa vijana hao walirudi nyumbani anapoishi kijana huyo ambaye anaishi na baba yake mzazi aliyejulikana kwa jina la Magee Saganda kisha kuitia moto nyumba moja na kuteketea kabisa.

Wanajeshi wa Jeshi la wananchi waliwahi kufika katika eneo la tukio na kuzuia uchomaji moto wa nyumba zingine ambazo nazo zilikuwa zinztaka kutiwa moto.

Mwandishi wa habari alifika katika eneo la tukio ambapo kwenye nyumba hiyo hapakuwepo na mtu yeyote yule lakini inadaiwa akina mama wa nyumba hiyo walipigwa na waendesha pikipiki hao na kukimbilia kusikojulikana.

Jeshi la polisi baada ya kufika lilichukua mwili wa marehemu na Balozi wa eneo hilo Peter Mabojano na baadhi ya wananchi wa kijiji hicho kwa ajili ya mahojiano zaidi.

Mwili wa marehemu umepelekwa katika Hospitali ya Mkoa huo na umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti kwa ajili ya taratibu za mazishi.

Tukio hili ni la tano kutokea katika wilaya ya Butiama ambapo katika matukio ya kuanzia Novemba mwaka jana hadi Februari mwaka huu ambapo matukio hayo ni kama ifuatavyo

Matukio hayo ni pamoja na la Desemba 21, mwaka huu saa 5:30 usiku Tabu Makanya (68) Mkazi wa Kijiji cha Kwikuba alichinjwa lakini watuhumiwa wakiwa katika harakati ya kuondoka na kichwa chake waliwahiwa na wananchi kisha kukitupa.

Lingine lilitokea Desemba 2,Blandina Peru alichinjwa na kuchukuliwa damu yake tu na Sabina Mkireri wa kijiji cha Kabegi, Kata alichinjwa na kuondoka na kichwa chake

Tukio jingine ni la kijana aliyetambuliwa kwa jina la Thomas Majengo (23-28) Mkazi wa Kiara Musoma Mjini alichijwa na kunyang'anywa pikipiki.


MWISHO





Read More...