Thursday, February 7, 2013

MAUAJI MENGINE BUTIAMA, WANAJESHI WAZUIA MAAFA








 Gari ya Jeshi la Polisi likiwa linatokea eneo la tukio la mauaji kijiji cha Etaro ambapo walichukua mwili wa marehemu Magere Masatu na kuupeleka Hospitali ya Mkoa wa Mara.
 Askari wa kutuliza ghasia wa Mkoa wa Mara wakiwa katika eneo la tukio kuzuia ghasia kutoka kwa waendesha pikipiki na wananchi wa kijiji cha Etaro wilaya ya Butiama
 Wananchi wa Kijiji cha Etaro wakiangalia nyumba ya Magee Saganda iliyochomwa moto baada ya mtoto wake Koti Magee kudaiwa kuhusika katika mauaji ya mwendesha pikipiki.
 Baiskeli zikiwa zimeungua ndani ya nyumba ya mtuhumiwa wa mauaji ya kijana Magere Masatu.
 wananchi wa Etaro wakishangaa tukio la uchomaji wa moto nyumba ya kijana anayetuhumiwa tukio la mauaji.


Na Thomas Dominick,
Butiama

MAUAJI ya kutisha bado yanaendelea kutokea katika Wilaya ya Butiama, Mkoa wa Mara baada ya kijana mmoja aliyetambulika kwa jina la Magere Masatu Mkazi wa Mtaa wa Nyakato, Wilaya ya Musoma kuuawa kasha kutupwa kwenye Mto wenye maji.

Katika tukio hilo Wanajeshi waliingilia kati na walifanikiwa kudhibiti maafa zaidi baada ya nyumba moja ya mtuhumiwa wa mauaji hayo kuchoma moto na kuteketeza kila kitu.

Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo wanadai kuwa tukio hilo lilitokea tarehe Februari 4 mwaka huu katika kijiji cha Etaro wilayani humo, ambapo walisema kuwa siku ya tukio marehemu aligongana na pikipiki na mwenzake ambaye akufahamika jina lake.

Walisema kuwa baada ya kugongana marehemu aliamua kumlipa fedha aliyegongana naye lakini balozi wa eneo la tukio alipelekewa pikipiki ya marehemu kwa ajili ya kuihifadhi.

“Baada ya tukio kweli pikipiki ilichukuliwa na kupelekwa kwa balozi wakati wanakwenda kuna vijana wawili walikuwa wakifuatilia kwa nyuma, na baada ya hapo marehemu hakuonekana tena hadi jana alipoonekana amekufa na yupo ndani ya mto,”alisema shuhuda aliyekataa kutaja jina lake.

Baada ya waendesha pikipiki wa Wilaya ya Musoma kupata taarifa kwa kuuwa kwa mwenzao walikwenda na kuvamia kijiji hicho kwa kuwapiga baadhi ya wananchi na balozi ambaye alikuwa amehifadhi pikipiki hiyo kisha kumtaja mmoja wa wauaji hao kuwa ni Koti Magee mkazi wa kijiji hicho.

Waendesha pikipiki hao walikwenda hadi kwa mtuhumiwa huyo na walimkuta lakini alifanikiwa kuwatoroka kisha kukimbilia ziwani na kujitosa kwenye maji kuogelea ikiwa ndio pona yake.

Baada ya kumkosa vijana hao walirudi nyumbani anapoishi kijana huyo ambaye anaishi na baba yake mzazi aliyejulikana kwa jina la Magee Saganda kisha kuitia moto nyumba moja na kuteketea kabisa.

Wanajeshi wa Jeshi la wananchi waliwahi kufika katika eneo la tukio na kuzuia uchomaji moto wa nyumba zingine ambazo nazo zilikuwa zinztaka kutiwa moto.

Mwandishi wa habari alifika katika eneo la tukio ambapo kwenye nyumba hiyo hapakuwepo na mtu yeyote yule lakini inadaiwa akina mama wa nyumba hiyo walipigwa na waendesha pikipiki hao na kukimbilia kusikojulikana.

Jeshi la polisi baada ya kufika lilichukua mwili wa marehemu na Balozi wa eneo hilo Peter Mabojano na baadhi ya wananchi wa kijiji hicho kwa ajili ya mahojiano zaidi.

Mwili wa marehemu umepelekwa katika Hospitali ya Mkoa huo na umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti kwa ajili ya taratibu za mazishi.

Tukio hili ni la tano kutokea katika wilaya ya Butiama ambapo katika matukio ya kuanzia Novemba mwaka jana hadi Februari mwaka huu ambapo matukio hayo ni kama ifuatavyo

Matukio hayo ni pamoja na la Desemba 21, mwaka huu saa 5:30 usiku Tabu Makanya (68) Mkazi wa Kijiji cha Kwikuba alichinjwa lakini watuhumiwa wakiwa katika harakati ya kuondoka na kichwa chake waliwahiwa na wananchi kisha kukitupa.

Lingine lilitokea Desemba 2,Blandina Peru alichinjwa na kuchukuliwa damu yake tu na Sabina Mkireri wa kijiji cha Kabegi, Kata alichinjwa na kuondoka na kichwa chake

Tukio jingine ni la kijana aliyetambuliwa kwa jina la Thomas Majengo (23-28) Mkazi wa Kiara Musoma Mjini alichijwa na kunyang'anywa pikipiki.


MWISHO





0 comments:

Post a Comment