Friday, December 28, 2012

JK AITAKA TAWIRI KUHAKIKISHA MBWAMWITU WALIOFUNGULIWA WANAKUWA SALAMA MUDA WOTE.







 Rais Kikwete akisalimiana na Mfugaji wa Mbwamwitu Joseph Kaboya ambaye aliwatunza kwa miezi miwili Mbwa hao walichukulia huko Loliondo kwa ajili ya kuja kuongeza Idadi ya wanyama hao ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti Mradi wa kwanza ulikuwa 30 Augosti mwaka huu ambapo Mbwamwitu 11 walitolewa na Mradi wa Pili ulikuwa Desemba 23 mwaka huu ambapo mbwamwitu 15 pia walitolewa.
 Rais Jakaya Kikwete akizungumza na waandishi wa habari katika Hifadhi ya Serengeti baada ya kufugua mradi ya pili wa Ufugaji wa Mbwamwitu 15 ambao wamefunguliwa kwa ajili ya kuongeza idadi ya wanyama hao katika hifadhi hiyo na kufikia 26, Mbwamwitu walipotea katika hifadhi hiyo miaka 1990 kutokana na magonjwa.
 Rais Kikwete akikata utepe kuashiria kuwa Mbwa mwitu 15 walifugwa ndani ya fansi hii baada ya kufugwa kwa miezi miwili ikiwa ni mkakati wa kuongeza wanyama hao ambao walipoea katika miaka 1990.
 JK akiwa na wajukuu zake mkono wake wa kulia wakiangalia jinsi Mbwamwitu (hawapo pichani) wakitoka ndani ya banda lao ambamo walikuwa wamefuygwa takribani kwa miezi miwili.

 Rais Kikwete akienda eneo lililotengwa maalumu kwa ajili ya kukata utepe kuashiria mradi wa awamu ya pili wa Mbwamwitutayari umekamilika na wapo tayari kufunguliwa na kuanza kuishi bila ya kufuygwa ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

Na Thomas Dominick,
Serengeti


RAIS Jakaya Kikwete ameitaka Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori
(TAWIRI) kuhakikisha Mbwamwitu waliofunguliwa rasmi katika mbuga ya Serengeti wanakuwa salama muda wote ili wasitoweke tena.


Mbwa hao waliochukuliwa eneo la Loliondo wamefugwa katika Hifadhi ya Taifa (TANAPA) kwa miezi mitatu hili likiwa ni kundi la pili lenye mbwamwitu 15 ambapo kundi la kwanza lilitolewa Agosti 30 mwaka huu likiwa na mbwamwitu 11 waliachiwa ndani ya hifadhi hiyo miaka ya 1980 ndani ya hifadhi hiyo kulikuwepo na mbwamwitu 500.


Kauli hiyo aliitoa mwishoni mwa wiki wakati wakiruhusu kundi la pili la mbwamwitu 15 ambao walikuwa wamefugwa katika eneo la Nyamuma ndani ya hifadhi hiyo kwa ajili ya juhudi za kuwarudisha wanyama hao ambao walitopotea miaka ya 1990.


“Sina shaka na mbwa hawa ila ninachowaomba ni kuwalinda na
kuwahakikishia usalama, ni miaka mingi sasa ndani ya hifadhi hii
hakuna mbwamwitu,”alisema Kikwete.


Rais Kikwete alisema kuwa kukosekana kwa wanyama hao ndani ya hifadhi hiyo kumesababisha kukosekana kwa kivutio kingine muhimu ambapo watalii wanahitaji kuwaona.


“Nawapongeza sana TAWIRI, Vodacom, TANAPA na mashirika yaliyofadhili mradi huu wa mbwa mwitu hii itasaidia kuongeza kivutio muhimu sana kwa watalii hata Ikulu nayo ilichangia milioni 30 kutokana na umuhimu wa mradi huu, hivyo natoa rai kwa mashirika mengine nchini kujitokeza kusaidia mradi huu ili kuweza kuongeza mbwa mwitu ndani ya hifadhi,”alisema.


Naye Mkurugenzi wa wa TAWIRI Dokta Simon Mduma alisema kuwa kutoweka kwa wanyama hao ni kutokana na magonjwa mbalimbali ya mbwa ambapo ililazimu kutoa chanjo kwa mbwa walioko karibu na hifadhi hiyo ili kuweza kumaliza magonjwa hayo na kuwarudisha mbwamwitu.


“Lengo letu ni kuleta familia sita ambazo zitapitia katika mradi huu
ili kuweza kuwaafya wasiweze kurudi kule walikotoka katika maeneo ya Loliondo na wazoee maisha ya hidfadhi ya TANAPA na waweze kuzaa na kuongezeka ili kiwe kivutio cha ndani ya hifadhi,”alisema Dokta Mduma.


Alisema kuwa kuna changamoto ambazo wanakabiliana nazo ikiwa ni pamoja mashirika mengi kutofadhili mradi huo ambapo kwa sasa kampuni ya simu za mikononi ya Vodacom ndio pekee iliyotoa ufadhili wa zaidi ya milioni 450.


Kutokana na kuruhusiwa kwa mbwamwitu hao sasa imeongeza na kufanya idadi ya wanyama hao kufikia 26 ndani ya TANAPA ambapo Agosti 30 mwaka huu waliachiwa 11 na mwishoni mwa wiki wameachiwa mbwamwitu 15.


MWISHO

0 comments:

Post a Comment