Tuesday, June 18, 2013

MAKILAGI CUP YAFUNGWA RASMI KATIKA KATA YA BWERI MANISPAA YA MUSOMA MKOANI MARA

 Katibu wa Umoja wa Vijana Wilaya ya (UVCCM)  Musoma Mjini Khalid King akiwa na Mfadhili ya Michuano ya Makilagi Cup ambaye ni Mbunge wa viti Maalum (CCM) Amina Makilagi wakiangalia fainali ya Ligi hiyo kati ya Machinjioni FC na Majengo FC ambao majengo FC waliibuka washindi kwa magoli 4-3 katika uwanja wa shule ya Sekondari ya Morembe. 
 Mbunge wa viti Maalum (CCM) Amina Makilagi akizungumza na timu ashindi na shiriki hawapo pichani kuhusu michuano hiyo na adhima yake ya kuboresha maisha ya vijana hao kwa kuwapatia fedha kwa ajili ya kujishughulisha katika kuinua kipato chao kwa kuanzisha vikundi vya ujasiliamali.
 Mbunge wa viti Maalum (CCM) Amina Makilagi akinyanyua Kombe juu kabla ya kuikabidhi timu bingwa ya majengo FC.
 Mbunge wa viti Maalum (CCM) Amina Makilagi akiwavisha medali wachezaji wa majengo FC ambayo ndio timu bingwa wa michuano ya Makilagi Cup.
 Timu ya Majengo FC wakiwa katika picha ya Pamoja huku kombe lao likiwa mbele.
 Mbunge wa viti Maalum (CCM) Amina Makilagi akikabidhi kombe kwa timu kapteni na kocha wa timu ya majengo FC.



Na Thomas Dominick,
Musoma

MASHINDANO ya Mpira wa miguu yaliyodhaminiwa na Mbunge wa Viti Maalumu  (CCM) na Katibu UWT Taifa Amina Makilagi yanayojulikana kama Makilagi Cup yamefika mwisho baada ya timu ya Majengo FC kuibuka washindi katika fainali iliyowakutanisha na timu ya Machinjioni FC zote za kata ya Bweri Manispaa ya Musoma Mkoa wa Mara.

Mchezo huo ulioanza majira ya saa kumi jioni katika viwanja vya shule
ya sekondari ya kutwa Molembe iliyopo katika kata ilishuhudiwa timu ya majengo FC wakiibamiza timu ya Machinjioni FC kwa magoli 4-3 katikia mchezo wa vuta nikuvute.

Wafungaji wa timu ya Majengo FC walikuwa ni Yohana Mirobo aliyefunga magoli mawili na Nyanda Rubeni naye aliyefunga magili mawili, na kwa upande wa machinjioni Fc magoli yalifungwa na Vicent Magesa, Adamu kulenga, Alex Andrew huku Vicent magesa akikosa penaiti dakika ya 89.

Baada ya mchezo huo Makilagi alikabidhi zawadi mbalimbali kwa
washiriki wa michuano hiyo ambapo timu ya nne na ya sita walizawadiwa pesa tasilimu sh. 50,000/=, timu yenye nidhamu ambayo ni Bweri FC walipata 50,000/=.

Mshindi wa tatu ambaye ilikuwa timu ya Victoria FC alizawadiwa sh.
200,000/=, mshindi wa pili mchinjioni FC walipata sh. 300,000/= na
mshindi wa kwanza ambaye ni Majengo FC walipata Kikombe, medali pamoja na fedha sh. 500,000/=.

Akifunga mashindano hayo Makilagi aliwaomba vijana hao wajiunge katika vikundi ili waweze kupata fedha kwa ajili ya kuanzisha miradi ya
maendeleo ambapo itawasaidia kukuza uchumi wao na wa Taifa.

"Mimi kama Mbunge ambaye nimetokea katika kata hii nimevutiwa sana na ninaguswa na matatizo yanayowakabili vijana hasa katika ajira na michezo hii imefungua ukurasa mpya kwenu nawaomba vijana wote mjiunge katika vikundi ili tuweze kuwasaidia kwa kuwapatia fedha kwa ajili ya miradi mbalimbali,"alisema makilagi.

Makilagi alisema kuwa ligi hiyo itakuwa ikichezwa kila baada ya miezi
sita huku shughuli za maendeleo kwa vijana hao zikiendelea kama
alivyowaahidi kuwa atawatafutia fedha kwa ajili ya maombi yao
waliyotoa kwa mbunge huyo.




Mwisho

Read More...

Saturday, June 15, 2013

MHUDUMU ATAKAYE UZA DAMU KWA MGONJWA ANAYEHITAJI DAMU KUCHUKULIWA HATUA ZA KISHERIA PAMOJA KUFUKUZWA KAZI.

 Mhudumu wa Damu salama akimchoma sindano kwa ajili ya kutoa damu Mwandishi wa Blog hii Thomas Dominick siku ya Maadhimisho ya Damu salama kitaifa ilifanyika Manispaa ya Musoma.
 Mwandishi wa habari wa Blog hii akitoa damu katika maadhimisho ya Damu salama Duniani ambapo kitaifa ilifanyika Manispaa ya Musoma Mkoani Mara.
 Naibu Waziri wa afya na Ustawi wa jamii Dkt. Seif Rashid akipata maelekezo toka kwa wahudumu wa Damu salama katika viwanja vya shule ya Msingi Mukendo Manispaa ya Musoma Mkoa wa Mara.
 Viongozi wa siasa waacha itikadi zao wamejumuika katika maadhimisho ya Damu Salama Mwenye suti ni Mkuu wa Wilaya ya Tarime John Henjewele, kushoto kwake ni Katibu wa CCm Wilaya ya Musoma Musa matoroka, na kulia kwake ni Christant Nyakitita Mwenyekiti wa Mkoa Chama cha DP na wa mwisho ni Elisha Erasto Katibu wa Mkoa wa chama UDP
 Dkt. Seif Rashid mwenye miwani akiangalia wacheza ngoma hawapo pichani siku ya maadhimisho ya Damu salama Duniani yaliyofanyika kitaifa Manispaa ya Musoma Mkoa wa Mara.
Mwakilishi wa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) Mkoa wa Mara, Emannuel Amas akipokea cheti maalumu kutoka kwa mgeni Rasmi  Dkt. Seif Rashid ikiwa kutambua mchango wa Televisheni katika kuhamasisha uchangiaji damu kwa hiari.



* Manispaa ya Musoma yavunja rekodi kwa kuchangia

*Vyombo vya habari vyatakiwa kuendelea kuhamasisha



Na Thomas Dominick,
Musoma
SERIKALI imesema kuwa haitasita kumchukulia hatua za kisheria pamoja na kumfukuza kazi mganga, muuguzi na mhudumu yeyote wa afya ambaye atabainika kuuza damu kwa mgonjwa anayehitaji damu.

Kauli hiyo ilitolewa na Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dokta Seif Rashid katika maadhimisho ya siku ya uchangiaji damu Duniani ambapo kitaifa ilifanyika Manispaa ya Musoma Mkoani Mara.

Katika takwimu za awali jumla ya chupa 5479 katika wilaya za mkoa huo zilikuwa zimeshachangiwa ambapo lengo lilikuwa kila wilaya ichangie chupa 600 ambapo zingekusanywa chupa 3600 lakini lengo hilo limevukwa.

Wakati zoezi la kuchangia likiendelea katika viwanja vya shule ya msingi Mkukendo manispaa ya Musoma ambapo ilidaiwa kuwa Manispaa ya Musoma iliongoza kwa kuchanfi chupa 1230, Tarime 1078, Butiama, 954, Rorya 874, Bunda 695 na Serengeti 648.

“Kwanza napenda kutoa wito kwa waganga, wauguzi na mhudumu yeyote wa afya ambaye atabainika kuuza damu kwa wagojwa ambao wanahitaji damu kuwa tukithibitisha kuwa ameshiriki kitendo hicho tutamchukulia hatua za kinidhamu pamoja na kumfukuza kazi,”alisema Dkt. Seif.

Katika hatua hiyo Dokta Seif aliwahamasisha wananchi  nchini kujitokeza kwa wingi kuchangia damu salama kwa ajili ya kuokoa maisha ya watanzania wenzao, hivyo wajitokeze katika vituo vya mpango wa Taifa wa damu salama au hospitali zilizo karibu.

“Kuchangia damu mara kwa mara kutasaidia kuwa na akiba ya damu ya kutosha hivyo kusaidia kupunguza kupunguza vifo ambavyo vinaweza kutokea kwa wagonjwa wanaohitaji damu kwa sababu ya ukosefu wa damu hospitalini,”alisema.

Alisema kuwa mikakati mbalimbali imewekwa kwa ajili ya kukabiliana na changamoto na kufikia malengo yake kwa kufanya kampeni ya uhamasishaji uchangiaji damu kwa hiari katika jamii.

Kuweka mikakati ya kujua matumizi halisi ya damu nchini na kuwakumbusha madaktari, wauguzi na wataalam wa maabara juu ya matumizi sahihi ya damu na kuendelea kuelimisha jami kwa kutumia vyombo vya habari, vipeperushi na kutumia vifungashio vya damu vyenye ujumbe vya DAMU HAIUZWI.

Pia alisema kuwa wizara inatoa rai kwa waganga wakuu wa mikoa kwa kushirikiana na halmashauri kutenga bajeti kwa ajili ya huduma za damu salama ikiwemo ukusanyaji wa damu katika mikoa na wilaya.

Vile vile alitoa rai kwa vyombo vya habari kuendelea kushirikiana na mpango wa Taifa damu salama katika kuhamasisha juu ya umuhimu wa kuchangia damu kwa hiari ili wananchi amba wamekuwa na imani potofu kuhusu kuchangia damu, wabadili imani zao na tabia ili nao waanze kuchangia.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Mara John Tuppa alitoa maombi kwa wizara hiyo kushirkiana ili kupanua uwezo wa kupima na kuhifadhi damu musoma badala ya kituo cha kanda kilichopo Mkoani Mwanza.

“Sio kama wizara ihamishe kituo cha mwanza bali hii itasaidia kuinua hamasa kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kuchangia damu ambayo wananchi wake watakapokuwa na mahitaji ya damu wasisubirie hadi kutoka mwanza,”alisema Tuppa.

Aliomba pia watoe adhabu stahili kwa kwa waganga, wauguz na wahudumu watakaobainika kuuuza damu kwa mgonjwa ambaye anahitaji damu ili kuokoa maisha yake.

Mwisho.
   

Read More...

Tuesday, June 11, 2013

AFISA MIPANGO MIJI AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA RUSHWA MKOANI MARA

Na Thomas Dominick,
Musoma.

TAASISI ya Kuzuia na kupambana na rushwa Mkoani Mara imewafikisha mahakamani na kuwafungulia shauri la jinai namba 97 ya mwaka 2013 Afisa Mipango Miji wa Halmashauri ya Manispaa ya Musoma kwa kupokea  rushwa.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari inadaiwa Afisa mipango miji aliyefikishwa mahakamani hapo Richard Maganga kwa kosa la kupokea rushwa ya shilingi Milioni 3.7 na David Mtae ambaye ni mwakilishi wa Lipaz Consultants ya Dar es Salaam kwa kutoa rushwa kinyume na kifungu 15(1)(a) na 15 (1)(b) cha sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa namba 11 ya 2007.

Mashitaka hayo ya kudai,  kupokea na kutoa rushwa yamefikishwa
mahakamani hapo mbele ya Hakimu Mkazi Ngigwana na mwendesha mashitaka wa TAKUKURU wakili Mwema Mella.

Akizungumza na waandishi wa habari Mkuu wa TAKUKURU Mkoa huo, Holle Makungu alieleza kwamba, afisa mipango huyo alipokea fedha hizo toka kwa mwakilishi wa kampuni hiyo inayojishughulisha na kutafuta maeneo ya vibali kwa ajili ya ujenzi wa minara ya simu.

Aidha Makungu alieleza kuwa mshitakiwa alipokea fedha hizo ili aweze kupitisha michoro na hatimaye kutoa vibali vya ujenzi wa minara hiyo vilivyokuwa vinaombwa kwa niaba ya kampuni ya AIRTEL na VODACOM.

Kesi hiyo imepangwa kutajwa tena Juni 25 mwaka huu na washitakiwa wote wawili wamerudishwa rumande kwa kushindwa kutimiza masharti ya dhamana ambayo ni wadhamini wawili wa kuaminika ambao wanatakiwa kuwa na mkataba na mahakama wa shilingi Milioni tano kila mmoja.

MWISHO
Read More...

ASKARI POLISI WAFUKUZWA KWA AIBU NA KUFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KOSA LA WIZI WA RISASI 1050

Na Thomas Dominick,
Musoma.

Jeshi la polisi mkoni Mara limewafukuza kazi kwa aibu na kuwafikisha Mahakamani askari wake wawili wanaodaiwa kukamatwa na risasi 1050 zinazodaiwa kuibwa kwenye kikosi cha kuzuia na kutuliza ghasia (FFU).

Askari ambao wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoa wa Mara ni askari aliyekuwa na cheo cha sajenti Michael Reus wa kikosi cha kutuliza ghasia mkoa wa Mara pamoja na askari mwenye cheo cha koplo Ally Machembe aliyekuwa akifanya kazi Kibaha mkoni Pwani.

Mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, ilielezwa na mwendesha mashitaka wa Serikali Jonas Kaijage mnamo juni mosi mwaka huu majira ya saa ya usiku askari hao walikamatwa kwenye basi la Mohamed Trans linalofanya safari zake kati ya Musoma na Dar es salaam wakiwa katika harakati za kusafirisha risasi hizo.

Ilielezwa Mahakamani hapo kuwa watuhumiwa wanakabiliwa na makosa matatu ikiwemo kosa la kula njama za kufanya wizi, kosa la pili kumwibia mwajiri wao kwenye kambi ya FFU na kosa la tatu ni kukutwa na risasi 1050 zinazotumika kwenye bunduki ya SMG na SR pasipokuwa na kibali.

Watuhumiwa hao walipelekwa Mahabusu baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana ambapo kila mmoja alitakiwa kuwa na dhamana ya shilingi milioni 5 na wadhamini wawili ambao ni watumishi wa Serikali.

Kesi ya askari ambao awali walifikishwa katika Mahakama ya kijeshi na kufukuzwa kazi kutokana na kutenda makosa hayo,kesi inayowakabili imepangwa kusikilizwa tena Juni 24.

Naye kamanda wa Polisi Mkoa wa mara Absalom Mwakyoma alisema kuwa kutokana na kutenda kwa makosa hayo Jeshi hili liliwafikisha katika mahakama ya kijeshi na kuwatia hatiani ambapo wote wawili wamefukuzwa kazi kasha kupelekwa mahakama ya kiraia.

“Tumewafukuza kwa aibu kutokana na makosa yao hayo ya kulidhalilisha jeshi letu kwani hatupo tayari kuona makosa kama hayo yakiendelea ambayo yanahatarisha usalama wa wananchi,”alisema Mwakyoma.

Inadaiwa askari huyo wa kikosi cha kutuliza ghasia (FFU) Mkoani Mara alikuwa katika Ghala la kuhifadhia silaha huenda alikuwa akijihusisha na biashara za kuuza silaha hali iliyopelekea kuwekwa kwa mtego huo ambao ulifanikiwa kumkamata.

MWISHO
Read More...

Wednesday, June 5, 2013

KAMPUNI YA AFRICAN BARRICK GOLD NORTH MARA WAKABIDHI HUNDI YA M. 10 KWA MWANDAAJI WA REDD'S MISS MARA 2013




 Washiriki wa Redd's Miss Mara wakiwa katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara wakisubiri kushuhudia ukabidhiwa kwa hundi ya M.10 kutoka Kampuni ya Madini ya African Barrick Gold North Mara.
 Kaimu Katibu Tawala Joseph Makingaakipokea hundi toka kwa Mratibu wa Huduma za jamii wa Kampuni ya Madini ya African Barrick Gold North Mara Fatuma Msumi.
 Kaimu Katibu Tawala Joseph Makingaakimkabidhi Mkurugenzi wa Homeland Intertainment and Promotion Godson Mkama
 Waandishi wa habari wakifanya mahojiano na washiriki wa Redd's miss Mara 2013.
 Waandishi wa habari wakifanya mahojiano na washiriki wa Redd's miss Mara 2013.
 Mkurugenzi wa Homeland Intertainment and Promotion Godson Mkama akifanya mahojiano na waandishi wa habari.
Washiriki wa Redd's Miss Mara wakiwa katika picha ya pamoja.



Na Thomas Dominick,
Musoma

Kampuni ya Madini ya African Barrick Gold North Mara umekabidhi fedha shilingi M. 10 kwa ajili ya ufadhili wake wa shindano la Redd's Miss Mara 2013.

Fedha hizo zilikabidhiwa mbele ya Kaimu Katibu Tawala Joseph Makinga na mbele ya waandishi wa habari wa Mkoa huo.

Makinga aliomba kampuni hiyo kuongeza udhamini mwakani ili mkoa uweze kufanya vizuri katika mashindano hayo kila mwaka pamoja na Chuo cha Musoma utalii kuongeza idadi ya washiriki wanaosoma katika chuo hicho toka watat hadi kumi.

Akikabidhi fedha hizo Mratibu wa Huduma za Jamii kutoka kwenye kampuni hiyo, Fatuma Msumi alisema kuwa wameamua kufadhili mashindano hayo tangu 2006 kwa ajili ya kurudisha fedha kwa jamii ya mkoa huo.

"Sisi tumekuwa tunatoa fedha kwa jamii kupitia miradi mbalimbali lakini kwa hili tumeamua kutoa fedha kupitia vipaji vyao ili kuwapatia uwezo wa kushinda katika mashindano makubwa ya kitaifa na dunia pia,"alisema.

Mwandaaji wa shindano hilo ambaye ni Mkurugenzi wa Home land Intertainment and Promotion, Godson Mkama ameshukuru kampuni hiyo kutoa kiasi hicho cha fedha na kusema kuwa wamejiandaa vyema kuhakikisha mshindi wa mwaka huu anauwakilisha mkoa huo vizuri.

"Lengo letu ni kufanya vizuri zaidi mwaka huu kuhakikisha tunashika nafasi ya kwanza redd's Miss Lake zone na Redd's Miss Tanzania,"alisema Mkama.

Washindani hao pia walisema kuwa shindano la mwaka huu ni gumu kutokana na washiriki wake kuwa ni warembo na wanajiamini kuliko miaka ya nyuma.

"Ninachoweza kusema kuwa shindano la mwaka huu ni gumu sana ukizingatia kila mshiriki amejiandaa vizuri sana na tunavutia mbele ya watu,"alisema Lilian Josephat mshiriki toka Wilaya ya Butiama.

MWISHO.



Read More...