Monday, November 26, 2012

CCM MUSOMA MJINI YAJIIMARISHA




 Mkereketwa wa CCM ambaye jina lake halikujulikana mara moja akiwa mbele ya maandamano ya wazee ambao walikuwa wanawasili katika viwanja vya Shule ya Msingi Mukendo kumsikiliza MNEC Vedastus Mathayo Kwenye Mkutano wa Hadhara wa Chama hicho.
  MNEC Vedastus Mathayo Akisalimia na wazee wa CCM Musoma Mjini wakati akiwasili kwenye mkutano hadhara
katika viwanja vya Shule ya Msingi Mukendo
 Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) wakifuatilia matukio yaliyokuwa yanaendelea katika viwanja vya Shule ya Msingi Mukendo Kutoka kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Musoma Mjini na MNEC Taifa Jackson Msome, katikati ni MNEC wa wilaya ya Butiama Christopher Marwa Siagi na kushoto ni MNEC Musoma Mjini Vedastus Mathayo.
 MNEC Musoma Mjini Vedastus Mathayo akiwahutubia mamia ya wananchi wa Musoma katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya shule ya msingi Mukendo.

 *Yafanya mkutano wa Kihistoria
*Chadema yaanza kubomolewa Musoma
*CCM yavuna wanachama 220
*Mamia ya wakazi wafurika viwanja vya Shule ya Msingi Mukendo

Na Thomas Dominick,
Musoma
                                                  
CHAMA cha Mapinduzi  (CCM) Wilaya ya Musoma Mjini Mkoa wa Mara kimevuna  wanachama 220 ambao wamekabidhiwa  kadi mpya na mjumbe wa Halmashauri Kuu Taifa  (NEC) Vedastus Mathayo huku kadi tano za CHADEMA zikirudishwa.

Wanachama hao walipatikana katika mkutano uliofanyika kwenye uwanja maarufu wa Shule ya Msingi Mkendo na kuhudhuriwa na mamia ya wakazi wa Wilaya hiyo .

Akihutubia katika Mkutano huo Mathayo alisema kuwa wamejipanga kuimarisha chama hicho kuanzia ngazi ya shina hadi Taifa ili kujihakikishia inashika dola katika uchaguzi mkuu utakaofanyika mwaka 2015.

“Katika kikao chetu kilichofanyika Dodoma chini ya Mwenyekiti wetu Rais Jakaya Kikwete tumejipangia kuboresha huduma za jamii hasa upande wa afya kwani tuna zahanati nyingi sasa tunataka tupate dawa za kutosha pamoja na wataamu wa afya kwa ajili ya wananchi wetu,”alisema Mathayo.

Alisema kuwa CCM baada ya uchaguzi wa ndani ya chama kinajikita zaidi katika kukiimarisha chama hicho na hatimaye kiibuke na ushindi katika chaguzi zijazo za serikali za mitaa ,rais,wabunge na madiwani .

Alisema kuwa kazi ya kubwa kwa sasa iliyo mbele yake ni kushughulikia matatizo  ya wanachama  katika wilaya yake kuhakikisha  ofisi zote za kata wilaya ya musoma zinang’aa na sambamba na kulikomboa jimbo la musoma mjini ambalo lilichukuliwa na chadema.

Alisema kuwa CHADEMA kimeshindwa kutekeleza ahadi walizojitoa katika uchaguzi mkuu na hivyo wakazi wa musoma kujuta kukichagua  cha hicho kilichojaa ahadi hewa lukuki .

“Tulikwisha waambieni wakati tunaomba ridhaa yenu ya kuongoza jimbo kuwa uongozi haujaribiwi sasa majibu mmeshayaona wenyewe tunachowaomba tushirikiane tulirudishe jimbo letu chini ya CCM ili wananchi wafaidi matunda ya chama chao,”alisema.

Alisema kuwa pamoja na kukichagua chama cha demokrasia na maendeleo wakazi wa musoma mjini hakuna kitu chochote  iliyotekelezwa na chama hicho ambapo mbunge wa jimbo la musoma vicent nyerere katika kampeni za kuwania ubunge aliahidi bwawa la kitaji litatoa gesi na badala yake limeendelea kuwa mazalia ya mbu.

Aidha amewaonya wanachama kuachana na makundi ambapo alisema binafsi yeye hataki makundi, hivyo wasahau yaliyopita katika chaguzi  na wagange yajayo
Baada ya hotuba hiyo wanachama 220 walijitokeza na kukabidhiwa kadi mpya za CCM huku  kadi tano za chadema zikirudishwa

Mwisho

0 comments:

Post a Comment