Friday, November 23, 2012

MNEC MATHAYO ACHANGIA ONGEZEKO LA AJIRA MKOANI MARA






 Mfanyakazi wa Kiwanda cha Mugango Ginnery akichuja mafuta ya kula yanayoitwa LADHA kabla ya kupimwa uzito na kufungwa kwa ajili ya mauzo.
 Gari likiwa tayari kwa ajili ya kupakia marobota ya pamba kwa ajili ya kusafirishwa nje ya mkoa huo.
 Mkurugenzi Joseph Mathayo maarufu Rambo akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya uzalishaji na utendaji kazi wa kiwanda hicho.
 Wafanyakazi wa kiwanda cha pamba wakitoka nje ya kiwanda baada ya kumaliza uzalishaji huku wakisubiria kuongeza kwa pamba kwa ajili ya kusindikwa.
 Mkurugenzi Joseph Mathayo maarufu Rambo (kushoto) akiwapa maelezo waandishi wa habari waliotembelea kiwandani hapo, kulia ni Augustine Mgendi nyuma ni Shomari Binda.
 Waandishi wa habari na Mkurugenzi wakiwa ndani ya kiwanda cha kusindika mafuta akitoa maelezo jinsi ya ushindikaji wa mafuta.
 Wafanyakazi wakiendelea na uzalishaji wa mafuta ndani ya kiwanda cha Mugango Ginnery kilichopo Wilaya ya Butiama.
 Hii ni nembo inayowakilisha bidhaa yake ya mafuta ambayo yanazalishwa na kiwanda hicho.
Paul Amon akipima uzito mafuta kwenye ndoo ya lita 20 kabla ya kufungwa na kuingizwa sokoni. 

*Ajira kuongezeka mwakani
*huzalisha zaidi ya lita 3000 kwa mpiko mmoja
*wakulima wasema ukombozi umewafikia 

Na Thomas Dominick,

Musoma



KIWANDA cha pamba cha Mugango Ginnery kinachomilikiwa na MNEC Vedastus Mathayo kinatarajiwa kuboreshwa miundombinu yake ili mwakani kitoe ajira nyingi kwa wakazi wa maeneo hayo.



Kiwanda hicho kilichopo katika kata ya Mugango wilaya ya Butiama, Mkoa wa Mara kwa mwaka huu kimetoa ajira za wananchi 175 ambao wanafanya kazi ndani ya kiwanda hicho ambacho kinazalisha mafuta ya kula, marobota ya pamba, pumba na mashudu kwa ajili ya mifugo.



Akizungumza na Waandishi wa habari kiwandani hao, Mkurugenzi Joseph Mathayo maarufu Rambo alisema kuwa wakati wanaanzisha kiwanda hicho walikutana na changamoto nyingi pamoja na kukuta miundombinu ikiwa imeharibiwa kabisa.



“Pamoja na kufanya kazi kubwa ya kuboresha miundombinu ambayo tumetumia pesa nyingi pia tulikutana na wakati mgumu wakati tunafuatilia vibali vya kazi kwa ajili ya kuanza ununuzi wa pamba,”alisema Mathayo.



Alisema kuwa tangu kiwanda hicho mahusiano na jamii inayowazunguka imeboreka zaidi kwa wakazi wa maeneo hayo wamekuwa wakipata misaada mingi ya kibinadamu pamoja na ajira ndani ya kiwanda hicho,”alisema.



Alisema kuwa kiwanda hicho kinazalisha zaidi ya lita 3000 kwa mpiko mmoja ambapokuna matanki mawili na kila tanki la mafuta linachukua lita 150.



Mathayo alitoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Mara na watanzania wanaotembelea mkoa huo kutokuwa na mashska na mafuta hayo kwa kuwa yanapikwa kwa ustadi mkubwa kulinganisha na viwanda vingine ambavyo vinatengeneza mafuta meusi.



“Ninachoweza kusema kuwa watanzania wasjaribu kuyatumia mafuta yetu waone radha yake kwani mafuta yetu ni meupe kuliko mengine kwa kuwa tuna wataalamu wa kutosha ambao wanafanya kazi zao kwa ustadi mkubwa sana,”alisema Mathayo.

Alisema kuwa kwa sasa mafuta hayo yanauzwa katika mikoa mitatu Mkoa wa Simiyu, Mwanza na Mara ambapo pia na bidhaa ya pamba inatoka katika mikoa hiyo hiyo.



Kuhusu suala la kuwasaidia wakulima zana za kilimo kama vile mbegu na mbolea ambapo wanawakopesha kwa kuandikiana na wakati wa manunuzi wanawakata fedha zao za pembejeo na madawa ya pamba.



Mmoja wa mkulima aliyejitambulisha kwa jina la Rajabu Juma mkazi wa Kijiji hicho cha Mugango alisema kuwa wanamshukuru mmiliki wa kiwanda hicho kutokana na mchango wake wa kuinua zao hilo ambalo lilianza kupoteza umaarufu nchini.



“Hatuna cha kumpatia lakini apokee shukurani zetu kwani sasa kilimo cha pamba amekirahisisha sana kwa kuwa tunapata mbegu kwa wakati pamoja na dawa zake hii inatutia moyo sisi wakulima,”alisema Juma.



Kiwanda hicho kilikuwa kinamilikiwa na vyama vya ushirika na kutelekezwa kwa miaka mingi hadi pale MNEC huyo alipoamua kukichukua na kuanza uzalishaji kwa mara ya kwanza mwaka huu.




0 comments:

Post a Comment