Wednesday, November 21, 2012

MAJAMBAZI YACHINJA YAIBA LAKI 1.76







 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara Absalom Mwakyoma akiandika kitu fulani kwa ajili ya kuwapatia waandishi wa habari hawapo pichani



Na Thomas  Dominick,
Musoma

MLINZI mmoja wa Kampuni ya ulinzi ya Salama Security  John
Nyaganya(22) ameuawa  kikatili kwa kuchinjwa shingo akiwa lindoni
katika eneo la Mkinyerero,barabara ya majita kata ya Kamunyonge
Manispaa ya Musoma Mkoa wa Mara.

Akizungumza na Habari Moto Moto Mara Ofisini kwake Jana  kamanda wa jeshi
la polisi mkoa wa Mara Absalom Mwakyoma alisema kuwa tukio hilo
limetokea  Alfajiri ya tarehe 21 mwaka huu.

Mwakyoma alisema  kuwa  alfajili hiyo mwili wa marehemu mlinzi wa
kampuni ya Samala security uligunduliwa  ukiwa umekatwa  shingo wakati
akiwa mwenye lindo la   la Pub ijulikanayo kwa jina la Pub ya Tulivu
mali ya mfanyabiashara mmoja  Paulo Karege(34) mkazi wa barabara ya
majita .

 Kamanda alisema kuwa  marehemu alikuwa ameajiliwa  na kampuni ya
Salama security  kulinda pub hiyo na uchunguzi  umeonesha kuwa  wauaji
hao walimuua kwa kutumia kitu chenye ncha kali na kasha  kuiba sanduku
 mbili za bia na viti vya plasitiki saba zenye thamani ya shilingi za
kitanzania 176,000/=.

 Alisema kuwa  ufatuliaji wa kina unafanyika  katika maeneo mbalimbali
ya   mji na nje ya mji ili kubaini waharifu hao  na kuwakamata ili
hatua za kisheria  zichukuliwe  haraka iwezekanayo.

Kamanda huyo aliongeza kuwa  mpaka sasa amekamatwa mtu mmoja (jina
limehifadhiwa kwa ajili ya uchunguzi) akiwa na nondo tatu,mtarimbo
,pinde na mishale mitatu,kirungu na nguo za kike.

Alisema wahalifu hao walikuwa wamevaa nguo za kike maarufu hijabu
(camouflage) ili kuficha sura ao wakati walipokuwa wakifanya kitendo
hicho na ametoa wito kwa wananchi kutoa taarifa  mara wanapoona watu
wanaowatilia mashaka pia amewataka kuimalisha vikundi vya ulinzi
shirikishi ili  kupunguza uharifu kwa wahalifu wengi wamo miongoni mwa
wananchi.


Mwisho.

0 comments:

Post a Comment