Monday, February 4, 2013

IMANI ZA KISHIRIKINA ZAMTOA UHAI

Na Thomas Dominick,
Musoma


MKAZI mmoja wa kijiji cha Nyiberekere kilichopo Wilaya ya Serengeti Mkoani Mara Nyabuke Maheri ,ameuawa kwa kupigwa mawe kisha kuchomwa moto kwa tuhuma za uchawi.

Kwa mujibu wa Taarifa kutoka kwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa huo, Absalom Mwakyoma,Bibi huyo mwenye umri wa miaka 68 alifikwa na mauti Februari 2 majira ya saa 10 jioni baada ya watu kadhaa kufika nyumbani kwake na kuubwaga mwili wa mtu aliyedaiwa kuuawa kichawi na bibi huyo Februari 1.

Watu hao wanaoelezwa kuwa wa ukoo mmoja na bibi huyo waliamua kujichukulia sheria mkononi baada ya marehemu Nyabunke kuwajibu kuwa hata wakimsusia maiti hiyo hawana uwezo wa kumfanya lolote.

Kamanda Mwakyoma alifafanua kuwa,hata hivyo mwili wa marehemu Kitene Kasinde(50)ulizikwa jana (feb 3)baada ya viongozi wa eneo hilo na jeshi la polisi kushauriana na ndugu hao kuondoa tofauti zao kwa kutoamani dhana ya uchawi na badala yake washirikiane kuusiri mwili huo.

Akizungumzia tabia ya wananchi kujichukulia sheria mkonono Mwakyoma ameapa kuwashughulikia ipasavyo wale wote wanaoendeleza tabia hiyo na kutoa wito kwa wanancho kushirikiana na kutoa taarifa kwa polisi pindi waonapo matukio ya aina hiyo.


MWISHO

0 comments:

Post a Comment