Monday, February 18, 2013

MEYA WA MANISPAA YA MUSOMA ANUSURIKA KUNG'OLEWA KATIKA MADARAKA YAKE.




 *Mwisho baada ya kuona imeshindikana wakatoboa siri 
* wasema mtego huo ulikuwa haumuachi madarakani
 *Mwenyekiti wa Chadema Mkoa ajikanyanga kwenye maelezo yake


 Diwani wa Kata ya Baruti Swaibu Mohamed (CCM) akitoa hoja kuhusiana kwa ukiukwaji kwa taratibu za kuwasilisha Bajeti ya Manispa ya Musoma ya Mwaka 2013/14, Bajeti hiyo iliwasilishwa Wizara ya Fedha bila kukaa kwa kamati za Manispaa hiyo kisha kupitishwa kwenye Kikao cha Madiwani.

 Diwani wa Kigera (CUF) Gabriel Ocharo akimbana Mkurugenzi wa Manispaa hiyo kwa madai ya ukiukwaji kwa taratibu za kuwasilisha Bajeti ya Manispa ya Musoma ya Mwaka 2013/14, Bajeti hiyo iliwasilishwa Wizara ya Fedha bila kukaa kwa kamati za Manispaa hiyo kisha kupitishwa kwenye Kikao cha Madiwani. 

 Angela Derrick Diwani wa Kata ya kamnyonge (CHADEMA) akieleza masikitiko yake yaliyofanywa na watendaji wa Manispaa ya Musoma kwa ukiukwaji kwa taratibu za kuwasilisha Bajeti ya Manispa ya Musoma ya Mwaka 2013/14, Bajeti hiyo iliwasilishwa Wizara ya Fedha bila kukaa kwa kamati za Manispaa hiyo kisha kupitishwa kwenye Kikao cha Madiwani. 

 Mkurugenzi wa Manispaa ya Musoma Ahmed Sawa akisoma na kutolea ufafanuzi wa kina uliosaidia kumnasua Meya wa Manispaa hiyo Alex Kisurura kung'olewa kwenye madaraka yake, Mkurugenzi huyo alieleza kuwa  waliamua kupeleka Bajeti ya Manispaa hiyo bila kupitia kwenye kamati husika kisha kwenye baraza la Madiwani ambapo madai yake makubwa yalikuwa ni kutokana na kubadilika kwa ratiba ya Bunge la bajeti ambalo litakaa Aprili mwaka huu badala ya Juni.



                                         Nyie wote ni mabwana wadogo hamuwezi kuning'oa ng'o!
 Mstahiki Meya wa Manispaa ya Musoma Akitoa maelezo yake baada ya kuona ameelemewa na madiwani kuhusiana na habari kuwa amehusika kusaini na kupeleka Bajeti ya Manispaa hiyo bila kufuata taratibu za kupitia kwanza kwenye Kamati za Manispa kisha kwenye baraza la madiwani.

Na Thomas Dominick
Musoma

MEYA wa Manispaa ya Musoma Mkoa wa Mara Alex Kisurura (Chadema) amenusurika katika mtego wa kung’olewa madarakani baada ya madiwani wa Manispaa hiyo kuitisha Baraza la dharura ili kujua kwa nini Rasimu ya Bajeti ya mwaka 2013/14 ilipelekwa hazina bila kufuata taratibu za Manispaa hiyo inayoongozwa na Chadema.

Kikao hicho kilichokaa mwishoni mwa wiki kuanzia saa 8 mchana hadi saa 11 jioni kilikuwa mikakati hiyo ilianza hivi karibuni baada ya kumtuhumu kuwa alishirikiana na Mkurugenzi wa Manispaa Ahmed Sawa kuwa wamepitisha na kusaini bajeti hiyo bila kufuata taratibu.

Mpango huo ulianza kuonekana baada ya wajumbe wa kamati mbalimbali kugoma kwenda kwenye vikao vya kutipia bajeti wakidai kuwa hawawezi kukaa hadi watakapoambia ni utaratibu gani umetumika kupitisha bajeti hiyo.

“Bajeti yetu lazima iwe ya uwazi na ilitakiwa ijadiliwe na kamati
mbalimbali kisha kuletwa kwenye kikao cha madiwani ili tuweze
kuipitisha kisha kwenda wizarani, sasa tunataka kujua ni taratibu gani zimepelekea bajeti hiyo kufika wizara ya fedha bila sisi madiwani kuja? Alihoji Angela Derrick Diwani wa Kamnyonge.

Baada ya vuta nikuvute ya hapa na pale huku Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, Sawa alitoa maelezo ya kina kwa kusema kuwa Serikali ilitoa maelekezo kuwa bajeti ya mwaka 2013/14 ilitakiwa kuwasilishwa Wizara ya fedha haraka iwezekanavyo kabla ya Januari 31 mwaka huu.

“Baada ya kupokea barua kuwa inatakiwa bajeti ya mwaka 2013/14 na muda uliobakia ni mdogo ilibidi tufanye haraka kukimbizana na muda na hii imetokana na mabadiliko ya kikao cha Bunge la bajeti ambalo litakaa mwezi Aprili mwaka huu,”alisema Sawa.

Mkurugenzi huyo alisema kuwa baada ya kuifikisha bajeti hiyo wizarani waliiomba wizara ya fedha kuwa hiyo iliyopelekwa sio bajeti kamili bali ni rasmu kutokana na kutopita kwenye kamati za Manispaa husika na kuomba kuwa bajeti kamili itapelekwa baada ya kukaa na kujadiliwa na kamati husika.

Alisema kuwa bajeti kamili inatakiwa kufikishwa hazina Februari 20 mwaka huu ambapo mkurugenzi huyo aliitisha vikao vya kamati mbalimbali lakini wajume  wake waligomea kuhudhuria vikao husika hadi watakapopata majibu ya kina.


Kutokana na maelezo marefu ya Mkurugenzi huyo madiwani walianza kuhoji kuwa nani aliyesaini bajeti ambapo hapo ndipo walipokuwa wanasubiria kuona kuwa Meya Kisurura kama amehusika kusaini ili mtego wao wa kumtimua utimie.

Baada ya kuzungusha huku na kule ndipo Diwani  Zeddy Sondobi akaamua kutoboa siri iliyojificha nyuma ya panzia kuwa ulikuwa umetegwa mtego ambao kama angehusika kusaini bajeti hiyo ukomo wa Umeya wake ungekuwa vumefika.

“Kwanza taarifa ya Meya ilikuwa inatuchanganya kuwa halmashauri zingine zilikaa kabla ya bajeti hiyo kupelekwa wizarani na tukawa tunaulizana bajeti yetu imeendaje bila kusainiwa tukajua lazima utakuwa umesaini na mtego wetu huu safari hii usingeruka,”alisema Sondobi Diwani wa Bweri.

Baada ya kikao hicho mwandishi wa Blog hii alimtafuta mwenyekiti wa Chadema Mkoa, Charles Kayele na kufanya naye mahojiano kuwa chama hicho kilifanya kikao cha siri ili kujadili suala hilo na kufikia maamuzi kuwa kama atakuwa ameshiriki kisiri kusaini bajeti hiyo ataondolewa nafasi hiyo.

“Hatukufanya kikao chochote kile ndani ya chama lakini tulikutana leo hii kabla ya kikao cha madiwani ambapo tulijadili sula hili na
kumuuliza meya kama ameshiriki katika kusaini bajeti hiyo ambapo
alikiri kuwa hakuusika na  wakati wa bajeti hiyo inaandaliwa alikuwa safirini Dar es salaam,”alisema Kayele.

Chama cha Demokrasia na Maendeo (CHADEMA) Manispaa ya musoma kimekuwa na mpasuko ndani ya chama hicho na migogoro ya hapa na pale ambapo wakati wameingia katika uchaguzi wa naibu Meya madiwani hao waliafikiana nafasi hiyo wampatie diwani wa CCM, ambapo mbunge wa  jimbo hilo Vicent Nyerere aliingilia kati na kumaliza tofauti hizo.

MWISHO

0 comments:

Post a Comment